IBADA NA MAZISHI YA MWANAHABARI CHARLES SOKORO WA BARMEDAS TV YAFANYIKA JIJINI MWANZA

Ibada ya Mazishi ya aliekuwa Mkuu wa Vipindi na Afisa Mahusiano katika kituo cha runinga cha Barmedas Tv cha Jijini Mwanza, Mwalimu Charles Sokoro, imefanyika jana katika Kanisa la AICT Makongoro na kufuatiwa na mazishi yaliyofanyika katika Makaburi ya Kitangiri.

Mwalimu Sokoro ambae pia alikuwa mwalimu wa muziki wa Injili na Mwenyekiti wa Kwaya ya AICT Makongoro, alifariki jumamosi Julai 16,2016 majira ya saa mbili usiku katika Hospitali ya Rufaa Bugando baada ya kuugua kwa miezi kadhaa.

Alizaliwa mwaka julai mosi mwaka 1965 katika Kijiji cha Kahunda Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza na hadi mauti yanamkuta alikuwa na umri wa 51 ambapo ameacha watoto wanne, alikuwa mgane.
Na BMG
Kwaya ya AICT Makongoro ikiimba katika ibada ya mazishi ya Sokoro
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la AICT Makongoro akitoa salamu za rambirambi katika ibada ya mazishi ya marehemu Sokoro.
Baba Askofu Mkuu Mstaafu wa Kanisa la AICT Makongoro, akitoa salamu za rambirambi katika ibada ya mazishi ya marehemu Sokoro.
Mmoja wawanafamilia wa marehemu Sokoro akisoma wasifu wa marehemu Sokoro.
Mchungaji Mika Ngusa kutoka TCRA akihubiri katika ibada ya mazishi ya marehemu Sokoro.
Jackson Manji Songo akiongoza ibada ya mazishi ya marehemu Sokoro
Mkurugenzi wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa Habari Tanzania, Abubakar Karsan, akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Wanahabari
Viongozi mbalimbali wa dini mkoani Mwanza, pamoja na waombolezaji wakiwa katika ibada ya marehemu Sokoro.
Viongozi mbalimbali wa dini mkoani Mwanza, pamoja na waombolezaji wakiwa katika ibada ya marehemu Sokoro.
Mratibu wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoani Mwanza, na mwanachama wa BMG Tanzania, Edwin Soko, pamoja na waombolezaji wakitoa wakiuaga mwili wa marehemu Sokoro

Haleluya Benjamin kutoka Mtandao wa Wanahabari Watoto mkoani Mwanza pamoja na waombolezaji wengine wakiuaga mwili wa marehemu Sokoro
Meneja wa Metro Fm ya Jijini Mwanza, na mwanachama wa BMG Tanzania, Alphonce Tonny Kapela, pamoja na waombolezaji wengine wakitoa wakiuaga mwili wa marehemu Sokoro
Baadhi ya wafanyakazi wa Barmedas Tv pamoja na waombolezaji wengine wakiwa katika mazishi ya mwalimu Sokoro
Mmoja wa watoto wa marehemu Sokoro (mwenye shati jeupe) akiwa na waombolezaji wengine katika mazishi ya Mwalimu Sokoro

Shangazi wa marehemu akimwaga udongo ishara ya kuuaga mwili wa marehemu Sokoro

Mkurugenzi wa Barmedas Tv akimwaga udongo ishara ya kuuaga mwili wa marehemu Sokoro

Baadhi ya Waandishi wa Habari wa kundi la Whatsupp la BMG Tanzania, wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Barmedas Tv

Post a Comment

أحدث أقدم