Ibada
ya Mazishi ya aliekuwa Mkuu wa Vipindi na Afisa Mahusiano katika kituo
cha runinga cha Barmedas Tv cha Jijini Mwanza, Mwalimu Charles Sokoro,
imefanyika jana katika Kanisa la AICT Makongoro na kufuatiwa na mazishi
yaliyofanyika katika Makaburi ya Kitangiri.
Mwalimu
Sokoro ambae pia alikuwa mwalimu wa muziki wa Injili na Mwenyekiti wa
Kwaya ya AICT Makongoro, alifariki jumamosi Julai 16,2016 majira ya saa
mbili usiku katika Hospitali ya Rufaa Bugando baada ya kuugua kwa miezi
kadhaa.
Alizaliwa
mwaka julai mosi mwaka 1965 katika Kijiji cha Kahunda Wilaya ya
Sengerema mkoani Mwanza na hadi mauti yanamkuta alikuwa na umri wa 51
ambapo ameacha watoto wanne, alikuwa mgane.
Na BMG
Kwaya ya AICT Makongoro ikiimba katika ibada ya mazishi ya Sokoro
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la AICT Makongoro akitoa salamu za rambirambi katika ibada ya mazishi ya marehemu Sokoro.
Baba Askofu Mkuu Mstaafu wa Kanisa la AICT Makongoro, akitoa salamu za rambirambi katika ibada ya mazishi ya marehemu Sokoro.
Mmoja wawanafamilia wa marehemu Sokoro akisoma wasifu wa marehemu Sokoro.
Mchungaji Mika Ngusa kutoka TCRA akihubiri katika ibada ya mazishi ya marehemu Sokoro.
Jackson Manji Songo akiongoza ibada ya mazishi ya marehemu Sokoro
Mkurugenzi
wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa Habari Tanzania, Abubakar Karsan,
akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Wanahabari
Viongozi mbalimbali wa dini mkoani Mwanza, pamoja na waombolezaji wakiwa katika ibada ya marehemu Sokoro.
Viongozi mbalimbali wa dini mkoani Mwanza, pamoja na waombolezaji wakiwa katika ibada ya marehemu Sokoro.
Mratibu
wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoani Mwanza, na mwanachama wa BMG
Tanzania, Edwin Soko, pamoja na waombolezaji wakitoa wakiuaga mwili wa
marehemu Sokoro
Haleluya
Benjamin kutoka Mtandao wa Wanahabari Watoto mkoani Mwanza pamoja na
waombolezaji wengine wakiuaga mwili wa marehemu Sokoro
Meneja
wa Metro Fm ya Jijini Mwanza, na mwanachama wa BMG Tanzania, Alphonce
Tonny Kapela, pamoja na waombolezaji wengine wakitoa wakiuaga mwili wa
marehemu Sokoro
Baadhi ya wafanyakazi wa Barmedas Tv pamoja na waombolezaji wengine wakiwa katika mazishi ya mwalimu Sokoro
Mmoja wa watoto wa marehemu Sokoro (mwenye shati jeupe) akiwa na waombolezaji wengine katika mazishi ya Mwalimu Sokoro
Shangazi wa marehemu akimwaga udongo ishara ya kuuaga mwili wa marehemu Sokoro
Mkurugenzi wa Barmedas Tv akimwaga udongo ishara ya kuuaga mwili wa marehemu Sokoro
Baadhi ya Waandishi wa Habari wa kundi la Whatsupp la BMG Tanzania, wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Barmedas Tv

إرسال تعليق