Pages

October 31, 2015

Full Time ya Simba Vs Maji Maji FC na matokeo ya mechi nyingine za Ligi Kuu October 31

Ligi Kuu Tanzania bara imeendelea tena leo October 31 kwa wekundu wa Msimbazi Simba kuwakaribisha Maji Maji FC wanalizombe kutokea Ruvuma Songea. Simba ambayo bado inatajwa kuwa hakuna mahusiano mazuri baina ya kocha Dylan Kerr na uongozi ambao inadaiwa wanaamini kuwa timu haipo katika kiwango kizuri.
DSC_0185
Ibrahim Ajib akijaribu kumtoka beki wa Maji Maji FC
Hata hivyo Simba waliingia uwanjani wakiwa na morali ya kutaka kupata ushindi kwani walifanikiwa kupata ushindi wa jumla ya goli 6-1, lakini kitu cha kuvutia ni pale ambapo wachezaji wa Simba walikuwa wakifunga na kwenda kushangilia na kocha wao kila goli, kitendo ambacho kilitafsiriwa kama kuonesha kuendelea kumkubali aendelee kuwepo katika timu.
DSC_0250
Nahodha wa Maji Maji FC Fred Mbuna akimdhibiti Ibrahim Ajib wa Simba katika eneo la hatari.
Magoli ya Simba yalifungwa na Ibrahim Ajib aliyefunga hat-trick kwa kuanza kufunga goli la kwanza dakika ya 8, 14 na 42 akakamilisha idadi ya goli zake tatu, Hamisi Kiiza alifunga goli mbili katika mchezo huo dakika ya 32 na dakika ya 81 baada ya dakika ya 71 Hussein Mohamed ‘Tshabalala’ kufunga goli la tano kwa Simba, Maji Maji FC walipata goli la kufutia machozi kupitia kwa Ditram Nchimbi.
Matokeo ya mechi nyingine za Ligi Kuu October 31
  • Kagera 0 – 2 Yanga
  • Coastal Union 1 – 1 Mbeya City
  •  Mtibwa Sugar 4 – 1 Mwadui FC
DSC_0216
Mwinyi Kazimoto akijaribu kumtoka beki wa Maji Maji FC
DSC_0317
Joseph Kimwaga akimtoka Fred Mbuna
DSC_0152
Wachezaji wa Simba wakimpongeza Ibrahim Ajib baada ya kufunga goli la kwanza
DSC_0179
Baada ya kufunga goli wachezaji wa Simba wakishangilia kwa pamoja na kocha wao Dylan Kerr
DSC_0325
Refa Alex Mahagi akimkabidhi mpira Ibrahim Ajib baada ya kufunga hat-trick
DSC_0137
Ndio siku ambayo Hamisi Kiiza alikabidhiwa hundi yake ya mchezaji bora wa mwezi na mdhamini wa Ligi.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...