Pages

February 27, 2015

BLOGGERS KUKUTANA JIJINI DAR KATIKA PATI YA KISTORIA


 Mwenyekiti wa Tanzania Bloggers Network  na mmiliki wa Blog ya The Habari.com Joachim Mushi (katikati) akizungumza wakati wa mkutano na waandishi. Kutoka kushoto ni  Mkala Fundikira,Shafia Mpanja wa AM,Ofisa Uhusiano wa NMB Doris Kilale na Khadija Kalili.
 Ofisa Uhusiano wa NMB Doris Kilale akifafanua jambo wakati wa mkutano.
 Mmiliki wa Blog ya Bongoweekeend Khadija Kalili akizungumza wakati wa mkutano.
 Father Kidevu (kulia) akifafanua jambo wakati wa mkutano.
Baadhi ya Bloggers na waandishi wa vyombo mbalimbali vya Habari wakifuatilia jambo wakati wa mkutano uliofanyika katika Ofisi za Idara ya Habari Maelezo Dar es Salaam.
Posted by MROKI On Friday, February 27, 2015 No comments

RAIS

KIKWETE

NA

MAKAMU

WAKE

WAAGA

MWILI

WA

MAMA

WA

DK

HOSEA

JIJINI

DAR

LEO







Posted by MROKI On Friday, February 27, 2015 No comments

WANANCHI

WA

MKOA

WA

NJOMBE

NI

MFANO

WA

KUIGWA

KATIKA

ZOEZI

LA

BVR

Kazi ya kuandikisha wananchi katika Daftari la Kudumu la Wapigakura kupitia mfumo wa Biometrick Voters Registration (BVR), ambao huhusisha uchukuaji wa alama za vidole na picha, jana iliingia siku ya tatu, huku baadhi yao wakipongeza utendaji wake.
Kwa mujibu wa ripoti iliyokusanywa na mwandishi wetu inasema kuwa tokea siku ya kwanza lilipoanza zoezi hilo lilionyesha matumaini maana wananchi wetu walijitokeza kwa wingi.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi katika vituo vya uandikishaji, wananchi hao walisema kuna mabadiliko ukilinganisha na siku zilizopita, hivi sasa kazi zinafanywa haraka.
“Watu wanaokwenda kwenye vituo kujiandikisha idadi yao ni kubwa kuliko hata makadirio ya tume, kama hawataongeza muda au vifaa, siku saba walizopanga, hazitatosha na wengi wataachwa bila ya kujiandikisha,” alisema.
Baadhi ya waandikishaji na wasimamizi wa mashine wameiomba Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) kuongeza muda ili kazi hiyo ifanyike kwa ufanisi zaidi.
66
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizindua  Uborereshaji wa Daftari kla Kudumu la Wapigakura  katika mji mdogo wa Makambako Februari 24, 2015. Kushoto ni Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Damian Lubuva na Katikati ni Katibu wa Tume hiyo, Ndugu Malaba.
02
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mwenyekititi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Damian Lubuva (kushpoto) , Naibu Katibu Mkuu  na Katibu Mwenezi wa CHADEMA, John Mnyika (kulia), Yusufu Mbungiro ambaye ni Afisa Uchaguzi na Mafunzo taifa wa Chama cha CUF (wapili kushoto) na Allan Bujo ambaye ni Mkuu wa Ulinzi wa CHADEMA baada ya kuzinua Uborereshaji wa Daftarila Kudumu la Wapigakura  katika mji mdogo wa Makambako.
03
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akitazama kazi ya uandiskishaji wapiga kura baada ya ya kuzinua Uborereshaji wa Daftari kla Kudumu la Wapigakura  katika mji mdogo wa Makambako.
 .06
Baadhi ya watalaamu wa kuandikisha wapiga  wakiwa na zana  za kazi kabla ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ya kuzindua Uborereshaji wa Daftari la Kudumu la Wapigakura  katika mji mdogo wa Makambako.
Posted by MROKI On Friday, February 27, 2015 No comments

NIC

WAKABIDHI

ZAWADI

ZA

WASHINDI

MASHINDANO

YA

LUGALO

CHALLENGE

CUP

4Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Shirika la Bima la Taifa NIC Bi. Mwanaidi Shemweta akikabidhi zawadi kwa Japhet Masai Kapteni wa mchezo wa Gofu katika viwanja vya gofu vya TPDF Lugalo tayari kwa mashindano ya NIC Corporate Lugalo Challenge 2015 yanayofanyika kesho February 28 kuanzaia saa 7:00 asubuhi kwenye viwanja hivyo yakishirikisha wachezaji mbalimbali kutoka ndani na nje ya Tanzania.
Mpaka sasa wachezaji 60 wameshathibitisha kushiriki katika mashindano hayo na wachezaji wengine wanaendelea kujisajiri ili kushiriki katika michezo hiyo ya Gofu, Kapteni Japhet Masai ametoa mwito kwa wachezaji mbalimbali kuendelea kujisajiri na amesema wanatarajia zaidi ya wachezaji 120 watashiriki katika mashindano hayo.
Shindano la NIC Corporate Golf Chalennge linaandaliwa na shirika la bima la taifa NIC na linafanyika kila mwaka kuanzia tangu lilipoanzishwa mwaka 2013 na linashirikisha wachezaji wa rika zote na jinsia zote NIC imeandaa zawadi mbalimbali kwa washindi, ambapo mshindi wa kwanza atapata jiko kubwa la umeme. Pia wshindi wengine watapata zawadi mbalimbali zilizotayarishwa kwa ajili yao ambazo ni meza kubwa ya ofisini, mikoba ya akina mama, mabegi ya wanafunzi, Feni , Friji, Microwave na zawadi nyingine nyingi.
 5Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Shirika la Bima la Taifa NIC Bi. Mwanaidi Shemweta akikabidhi zawadi kwa ya jiko kubwa la umeme Japhet Masai Kapteni wa mchezo wa Gofu katika viwanja vya gofu vya TPDF Lugalo.
 6Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Shirika la Bima la Taifa NIC Bi. Mwanaidi Shemweta na Japhet Masai Kapteni wa mchezo wa Gofu katika viwanja vya gofu vya TPDF Lugalo wakipiga picha pamoja na zawadi hizo.
 7Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Shirika la Bima la Taifa NIC Bi. Mwanaidi Shemweta akipiga picha mara baada ya kukabidhi zawadi hizo kwenye viwanja vya gofu vya TPDF Lugalo.
Posted by MROKI On Friday, February 27, 2015 No comments

SOMA

JARIDA

LA

WIKI

LA

NISHATI

NA

MADINI,

TOLEO

LA

56

Posted by MROKI On Friday, February 27, 2015 No comments

MKAZI

WA

DODOMA

JELA

MAISHA

KWA

KUNAJISNI

Tarehe 24/02/2015 katika Mahakama ya Wilaya ya Mpwapwa Mkoa wa Dodoma, mtu mmoja anayefahamika kwa jina la YUSUPH CHATAMBALA, umri miaka 45, kabila Mchaga, Mkulima na mkazi wa Kijiji cha MAKUTUPA Kata ya Lupeta Wilayani Mpwapwa Mkoa wa Dodoma, amehukumiwa kifungo cha maisha jela kwa kosa la KUNAJISI mtoto wa miaka mine (4).


Mwendesha Mashitaka wa Polisi katika Mahakama ya Wilaya ya Mpwapwa Mkaguzi Msaidizi wa Polisi  GODWILL S. IKEMA (A/Insp) akisoma mashitaka Mahakamani alisema, Mtuhumiwa alitenda kosa la KUBAKA lililo kinyume cha sheria za nchi chini ya Kifungu namba 130 (1) 2 (a) na 131 (1) cha Kanuni ya Adhabu kama kilivyofanyiwa mapitio mwaka 2002. 
YUSUPH CHATAMBALA alitenda kosa hilo siku ya tarehe 20/02/2015 saa 12:00 jioni, huko kijiji cha Makutupa Wilaya ya Mpwapwa Mkoa wa Dodoma, ambapo alimbaka mtoto mdogo wa kike mwenye miaka 04 (jina limehifadhiwa). Alitenda kosa hilo baada ya kumkamata alipokuwa akicheza na watoto wenzake jirani na nyumbani kwao kisha kumpeleka kwenye shamba la mahindi kisha KUMNAJISI mtoto huyo na kusababishia majeraha na maumivu makali.


Mtuhumiwa alifikishwa mahakamani siku ya tarehe 23/02/2015 na kusomewa shitaka lake, ambapo alikiri kutenda kosa hilo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya ya Wilaya ya Mpwapwa Mh. PASCHAL F. MAYUMBA. Siku ya tarehe 24/02/2015 alifikishwa tena Mahakamani hapo na kusomewa tena shitaka lake na kukiri tena kutenda kosa hilo.


Hakimu Mkazi  Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpwapwa Mh. PASCHAL  F. MAYUMBA alimtia hatiani mtuhumiwa huyo baada ya kukiri kutenda kosa hilo. Akisoma hukumu hiyo; Mh. Hakimu Mkazi Mfawidhi,  alisema Mahakama inamhukumu kwenda Jela Kifungo cha Maisha kwa kosa la Kumnajisi mtoto ili kuwa fundisho kwake na kwa wengine wanaotenda makosa kama hayo.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi D. A. MISIME – SACP alithibitisha kuwepo kwa tukio hilo na hukumu iliyotolewa dhidi ya mtuhumiwa huyo. Kamanda Misime alisema Makosa ya Unyanyasaji wa Kijinsia yamekuwa yakichukuliwa hatua kali kutokana na uelewa wa wananchi juu ya ubaya wa vitendo vinavyofanywa na kutolea taarifa bila woga katika Madawati yanayoshughulikia kesi hizo katika vituo vya Polisi. Alisisitiza kuwa wananchi waendelee kushirikiana na Jeshi la Polisi kuwafichue wahalifu wa makosa yote na kuyafanya makazi yao kuwa sehemu salama ya kuishi na kujiletea maendeleo bila hofu dhidi ya wahalifu.


Imetolewa na Idara ya Habari na Matukio Polisi Mkoa wa Dodoma.
KNY: Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma 
Picha iliyotumika ni ya Gereza Kuu la Kigali Nchini Rwanda
Posted by MROKI On Thursday, February 26, 2015 No comments

PATO

LA

TAIFA

LAONGEZEKA,

LAFIKIA

SHILINGI

TRILIONI

Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Bw. Morrice Oyuke (Kulia)akitoa taarifa ya Pato la Taifa kwa kipindi cha robo tatu ya mwaka 2014 leo jiji Dar es salaam. Pato hilo kwa mwaka 2014 limefikia kiasi shilingi trilioni 21.2  kutoka trilioni 19.8 za mwaka 2013, Kushoto ni  Mtakwimu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Gregory Milinga,
Pato la Taifa (GDP)  katika kipindi cha robo ya tatu ya mwaka 2014 limeongezeka hadi kufikia shilingi trilioni 21.2  kutoka shilingi trilioni 19.8  za kipindi kama hicho kwa mwaka 2013.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jiji Dar es salaam, Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Bw. Morrice Oyuke, amesema kuwa katika kipindi cha robo tatu ya mwaka 2014 sekta nyingi za uchumi zimefanya vizuri katika uzalishaji ikilinganishwa na mwaka 2013.

Amesema katika kipindi hicho shughuli za uchimbaji wa Madini , Mawe na Kokoto zimekua kwa asilimia 5.2 ikilinganishwa na asilimia 3.3 za mwaka 2013, Uzalishaji wa bidhaa za viwandani  ukikua kwa asilimia 10.8 kutoka asilimia 10.4 pamoja na ongezeko la uzalishaji wa umeme kwa asilimia 10.7 kutoka asilimia 10.3 za mwaka 2013 kutokana na matumizi ya mafuta na Gesi.

Amezitaja sekta nyingine kuwa ni usambazaji maji ambao umekua kwa asilimia 12.7 kutoka 6.9 za mwaka 2013, Habari na Mawasiliano kwa asilimia 11.9 kutoka 7.0, Shughuli za Fedha na Bima zikikua hadi kufikia asilimia 13.9 kutoka asilimia 6.8 za mwaka 2013.

Ameongeza  kuwa  katika kipindi hicho huduma za upangishaji wa nyumba zilikua  hadi kufikia asilimia  2.2 kutoka 2.1,  shughuli za kitaalamu, kisayansi, ufundi na utawala  zikifikia  asilimia 5.4 kutoka asilimia 1.0 ya mwaka 2013.

 Bw. Oyuke amezitaja  shughuli  nyingine kuwa ni uendeshaji wa Serikali ambazo zilikua  kwa asilimia 4.9 ikilinganishwa na 4.4, huduma za Elimu kwa asilimia 3.7 kutoka 3.5, Afya kwa asilimia 8.1 pamoja na shughuli za Sanaa na Michezo ambazo zilikua kwa asilimia 2.5 ikilinganishwa na 1.6 ya mwaka 2013.

Aidha, amebainisha kuwa uzalishaji wa Almasi katika kipindi cha robo tatu ya mwaka 2014 ulikuwa karatasi 66,508 ikilinganishwa na karatsi 27,828 zilizozalishwa katika kipindi kama hicho mwaka 2013.

Akizungumza kuhusu sekta ambazo hazikufanya vizuri katika kipindi cha Robo tatu ya mwaka 2014 Mkurugenzi huyo amesema kuwa  ni dhahabu  ambayo uzalishaji wake ulifikia Kilogramu 10,137 kwa mwaka 2014 ikilinganishwa na 11,010 za mwaka 2013,Madini ya Tanzanite kilogramu 1,449 kutoka 5140 zilizozalishwa mwaka 2013.

Amefafanua kuwa shughuli za Biashara za Jumla na reja reja, Ukarabati wa magari na pikipiki pamoja na vifaa vingine vya nyumbani zimeonyesha kukua kwa asilimia 6.0 kwa mwaka 2014 ikilinganishwa na kasi ya asilimia 6.7 ya mwaka 2013, shughuli za uhifadhi asilimia 13.9 kwa mwaka 2014 ikilinganishwa na asilimia 19.3 za mwaka 2013.

Aidha, amebainisha kuwa katika kipindi hicho cha miezi mitatu ya mwaka 2014 kuanzia Julai mpaka Septemba, Pato la taifa kwa bei za mwaka 2007 limefikia kiasi cha Shilingi trilioni 10. 7 ikilinganishwa na shilingi trilioni 10.1 ya mwaka 2013.
Posted by MROKI On Thursday, February 26, 2015 No comments

MANISPAA

YA

TEMEKE

YA

MWAGA

KINYESI

ALICHO

HIFADHI

MWALIMU

WA

KIBASILA

CHUMBANI

Ama kweli ukistaajabu ya musa hakika utayaona ya firauni...na kuishi kwingi ni kuona mengi...hali kadhalika wahenga wanasema Tembea uyaone...Misemo hiyo mitatu inaweza kujidhihirisha kwa namna tofauti tofauti kupitia tukio la mkazi wa Jiji la Dar es salaam ambaye ni Mwalimu wa kike katika shule ya Sekondari Kibasila iliyopo hatua kadhaa kutoka Manispaa ya Temeke kubainika ndani kwake alipokua akiishi huko Yombo, Kisiwani Kata ya Sandari kuwa kuna shehena ya kinyesi cha binadamu katika ndoo, mabeseni, chupa za soda, maji pamoja na majagi.
Pichani juu ni  Wafanyakazi wa usafi wa Manispaa ya Temeke wakibeba kinyesi kwenda kukimwaga baada ya kuvunja nyumba aliyokuwa akiishi Mwalimu Gaudencia Albert.
 Ubebabi kinyesi ukiendelea
Shehena ya kinyesi iliyokuwa chumbani kwa mwalimu huyo. 


 ********
Manispaa ya Temeke jana Februari 25, 2015, imeteketeza kinyesi kilichokutwa katika chumba cha mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Kibasila Gaudensia Albert baada ya maofisa wa afya wa manispaa hiyo kuchukua hatua hiyo ili kunusuru afya za wakazi wa eneo hilo.
Kazi hiyo ilifanyika majira ya saa tisa alasiri katika eneo la Yombo, Kisiwani Kata ya Sandari jijini Dar es chini ya uangalizi wa Jeshi la Polisi na wakishirikiana na Mwanyekiti wa Mtaa huo, Yahya Bwanga.
Akizungumza na wandishi wa habari jijini wakati wa zoezi hilo, Ofisa Afya wa Manispaa ya Temeke, Floyd Tembo alisema tukio hilo walilipata juzi juzi jioni, baada ya kulipata waliwatuma Watendaji wa Afya wa Kata hiyo wafanye utafiti wakujua tatizo hilo lilikuwa na ukubwa gani. SOMA ZAIDI KWA KUBOFYA HABARI MSETO BLOG
Posted by MROKI On Thursday, February 26, 2015 No comments

CHID

BENZ

ALIPA

FAINI

900,000/=,

AACHIWA

HURU

NA

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu leo imemwachia mwanamuziki Rashid Makwilo 'Chid Benz' baada ya kulipa faini ya sh. 900,000 kufuatia kukamatwa akiwa na madawa ya kulevya.
 
Chid Benz alikamatwa mwaka jana katika Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam akiwa na madawa ya kulevya, ikiwemo misokoto ya bangi.
Mwanamuziki huyo ambaye alikiri kosa hilo wiki iliyopita, alikamatwa uwanjani hapo akiwa anajitayarisha kupanda ndege kwenda Mbeya kwenye tamasha la muziki.
CHIDI BENZ HURU:Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo imemwachia mwanamuziki 'Chid Benz' baada ya kulipa faini ya 900,000/= kwa kukutwa na madawa ya kulevya. SOURCE: GPL
Posted by MROKI On Thursday, February 26, 2015 No comments

Tamthilia

ya

"A

Boys

Mission"

yahitaji

Milioni

800

ili

 Mwenyekiti Mtendaji wa kampuni ya Forward Formidable Enterprises (FFE) inayoandaa tamthilia mpya na ya kisasa ya “A boys mission” Johnson Lujwangana akifafanua jambo kuhusiana na tamthilia hiyo itakayoanza kurushwa kwenye vituo vya televisheni kuanzia mwezi septemba. Wengine katika picha kutoka kulia ni Jesca haule na Aisha bakari.
Mwenyekiti Mtendaji wa kampuni ya Forward Formidable Enterprises (FFE) inayoandaa tamthilia mpya na ya kisasa ya “A boys mission” Johnson Lujwangana katikati akifafanua jambo kuhusiana na tamthilia hiyo itakayoanza kurushwa kwenye vituo vya televisheni kuanzia mwezi septemba. Wengine katika picha kutoka kushoto ni Brian daniel, Neema Mung'anya, Samuel katabazi, Jesca haule, Aisha bakari na Victor Casmir.
 
 Waigizaji wa tamthilia ya “A boys mission” inayoandaliwa na kampuni ya Forward Formidable Enterprises katika picha ya pamoja.
  *****
Kampuni mpya katika utengenezaji wa filamu nchini, Forward Formidable Enterprises (FFE) inayoandaa tamthilia mpya na ya kisasa ya “A boys mission” inahitaji kiasi cha Sh milioni 800 ili ikamilike.

Mwenyekiti Mtendaji wa kampuni ya FFE, Johnson Lujwangana alisema kuwa kwa sasa wameweza kutengeneza toleo la utangulizi "pilot episode' kwa ajili ya kuonyesha nini wanakifanya huku kila kitu kikiwa tayari kwa ajili ya kurekodiwa. Johnson alisema kuwa tamthilia yao inazungumzia changamoto na suluhisho mbalimbali kwa maisha ya vijana nchini na fedha hizo zinahitajika kwa ajili ya kughalimia gharama mbalimbali za kuzalisha rasmi tamthilia hiyo.

Baadhi ya gharama hizo kwa mujibu wa Johnson ni kulipa mtayarishaji bora, kuwalipa wasanii fedha kutokana na ubora wa kazi zao, kulipia vifaa vya kisasa, kulipa sehemu bora ya kurekodi tamthilia, usafiri, chakula na gharama nyinginezo.

“Kama msanii wa muziki wa kizazi kipya, Diamond anatengeneza video ya dakika tatu kwa Sh Milioni 60, kwa nini tamthilia ambayo kila sehemu (episode) inatumia si chini ya dakika 45 hisifikia kiwango hicho cha fedha? Alihoji Johnson. Alisema kuwa wao wanataka kuwafaidisha wasanii wao kwa kuwalipa vizuri na kuendelea kudumu katika fani na kuwataka wadhamini kujitokeza kwa wingi kusaidia mradi huo.

“Hakuna hata msanii mmoja maarufu katika tamthilia hii, lengo si kama kuwatupa wasanii hao, bali ni kupanua wigo na kuwapa nafasi wasanii wengine, nataka kizazi kipya zaidi katika tasnia ili kuendeleza kuzalisha mastaa,” alisema. Alisema kuwa katika tamthilia imeonyesha na kutoa majibu ya nini vijana wanatakiwa kufanya hapa nchini na kuachana na fikra za kukimbilia nje ya nchi  kwa kudhani kuwa ndiko kutakuwa suluhisho la matatizo yao.

Alifafanua kuwa mara baada ya kufika huko, hali inakuwa tofauti na kukutana na changamoto nyingi zaidi za maisha na kuwaza kurejea nchini. “Tamthilia ni ya kisasa zaidi kwani lengo letu pia ni kuonyeshwa nje ya nchi na kuonyesha madhari ya kuvutia ya jiji letu la Dar es Salaam na kupromoti mji wetu tofauti na hali iliyozoeleka kwani tamthilia nyingi uonyesha maisha ya vijijini,” alisema Johnson.

Alifafanua kuwa kwa kuonyesha usafi wa mji, maeneo mbalimbali ya starehe ya hapa nchini, kutawavutia hata wasanii watayarishaji wa tamthilia nje ya nchi kuja kutayarishia kazi zao hapa nchini. Alisema kuwa tamthilia hiyo ina jumla ya sehemu 12 ambapo katika kila sehemu, muigizaji mkuu ma maudhui ya tamthilia pia yanabadilika.
Posted by MROKI On Thursday, February 26, 2015 No comments

ZIARA

YA

WAZIRI

MKUU

PINDA

MBEYA

MJINI

NA

MBEYA

5
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiweka jiwe la Msingi la zahanati ya Kimondo , Mbeya Vijijini akiwa katika ziara ya mkoa  wa Mbeya, Februari 25, 2015. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Mjini Dr. Norman Sigalla.
4
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwapungia wananchi wa Kijiji cha Kimondo, Mbeya Vijijini  kabla ya kuweka jiwe la Msingi la zahanati yao akiwa katika ziara ya mkoa wa Mbeya Februari 25, 2015. Kushoto kwake ni Mbunge wa Mbeya Vijijini, Luckson Mwanjale na kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Mbeya mjini Dr. Norman Sigalla.
3
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikagua soko Kuu la Mjini Mbeya la Mwanjelwa baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wake akiwa katika ziara ya mkoa wa Mbeya, Februari 25, 2015.
2
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwasikiliza wanafunzi wa shule ya sekondari ya Iwambe mjini Mbeya wakati alipofungua na kukagua maabara tatu za shule hiyo akiwa katika ziara ya mkoa wa Mbeaya Februari 25, 2015. Kushoto ni mkewe  Tunu. 
6
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na wananchi baada ya kufungua vyumba vitatu vya Maabara katika shule ya sekondari ya Songwe mkoani Mbeya Febrari 25, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
9
Max Oswald (kushoto) na  Ivan Kina wakitumbuiza katika mkutano wa hadhara  uliohutubiwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika kijiji cha Igoma , Mbeya Vijijini Februari 25, 2015.
Posted by MROKI On Thursday, February 26, 2015 1 comment

SHULE

ZA

MSINGI

MKOANI

SINGIDA

KUPOKEA

VITABU

Miss Singida na Miss Kanda ya Kati 2014/15 ,Doris Mollel akisikiliza jambo kutoka kwa Afisa Mipango wa Children’s Book Project for Tanzania,Ramadhani Ali wakati akipokea vitabu kutoka Children’s Book Project for Tanzania.
*********
SHULE tatu za msingi katika mkoa wa Singida,zitapokea vitabu 200 wiki hii kusaidia katika mchakato wa kuboresha elimu ya shule ya msingi. Vitabu hivi vimetolewa na taasisi isiyo ya kiserikali ya Children’s Book Project for Tanzania na italenga maelfu ya watoto nchini kote katika kuwakomboa kielimu.

Akizungumza wakati wa kukabidhi vitabu hivyo,Afisa Mipango wa Children’s Book Project for Tanzania,Ramadhani Ali alisema kuwa Watoto wanaotakiwa kupata vitabu hivi ni wale walio na uhitaji sana na watapata nafasi ya kunufaika zaidi kielimu.

"Watoto wanaopata vitabu hivi ni wale walio na uhitaji sana na watapata nafasi ya kunufaika zaidi kielimu. vitabu hivi vinatolewa kwa watoto ili waweze kutumia katika masoma yao ya kila siku shuleni.” alisema Ramadhani

Msaada huu wa vitabu umejikita katika kukomboa hali ya elimu Tanzania, huku serikali ikijitahidi kuwekaza katika elimu nchini kwa kipindi kirefu. Inakadiriwa kuwa asilimia kubwa ya watoto wa shule ya msingi Tanzania hawajui kusoma na kuandika,Ukosefu wa vitabu unachangia wanafunzi wa shule ya msingi kushindwa kusoma na kuandika.

Tafiti mbalimbali kutoka za serikali na sekta binafsi zinaonyesha wazi kuwa kujifunza kusoma mapema ni uwekezaji katika siku zijazo kwa mtoto,kwani elimu katika ngazi ya chini kwa mwanafunzi inachangia kuboresha maisha yake ya baadae.

Kwa upande wake Doris Mollel ambaye ni Balozi wa Elimu mkoani Singida anatambua umuhimu wa elimu katika ngazi ya chini na anatumia muda wake mwingi katika harakati za kukomboa elimu ya shule ya msingi. Ziara zake nyingi hujikita katika mikoa ya ukanda wa kati hususani Singida na Tanzania kwa ujumla,Vile vile ni mshauri wa wanafunzi wa shule za msingi.

"Msingi wa kujifunza kusoma hufungua uwezo wa kufikiri kwa mwanafunzi akiwa na umri mdogo bila kiini hiki cha msingi maendeleo na mafanikio ya mwanafunzi ni magumu.” alisema Doris

Doris Mollel ni Miss Singida kanda ya kati 2014/15 na analenga katika kuboresha maisha ya jamii kwa kupitia elimu na masuala mengine ya kitamaduni.
Posted by MROKI On Wednesday, February 25, 2015 No comments

ATUHUMU

POLISI

KUMVUNJA

MKAZI wa Loksale wilaya ya Monduli, Samwel Petro Shani(47) amelalamikia hatua ya kuvunjwa mikono yake miwili kwa kipigo cha askari polisi katika kituo cha Leskale kwa madai ya kushindwa kulipa deni ya shilingi 250,000 alizokuwa akidaiwa ana mfanyabiashara wa eneo hilo.

Aidha anawatuhumi askari hao kukodiwa na mfanyabiashara mmoja mkazi wa eneo hilo kwa lengo la kumshikisha adabu baada ya mkazi huyo kushindwa
kulipa deni la sh,250,000  alizokuwa akidaiwa na mfanyabiashara huyo.
 
Samweli ameeleza kupokea kipigo hicho ambapo alidai kuwa dhamira ya askari hao ilikuwa ni kumtoa uhai wake kwani walikuwa wakitumia chuma kinene kumpiga na kumvunja mikono yake miwili huku mwingine alikuwa akimshambulia kwa runngu na mateke.

Akizungumza kwa majonzi na gazeti hili jijini hapa,alieleza kuteswa na askari hao wanaodaiwa kukodiwa na mfanyabiashara aliyemtaja kwa jina moja la bi Shamimu,ambaye alikuwa akimdai kiasi hicho cha fedha.

Alieleza kuwa tukio hilo lilitokea februali 6,mwaka huu majira ya saa 3 usiku na kwamba aliwatambua askari wawili waliomtesa kwa kipigo kuwa ni Steven na Justini wote ni askari wa kituo hicho cha Loksale.

''Mnamo tarehe 6 mwezi huu majira ya saa 3 usiku,walikuja askari wawili wakiwa wamevaa nguo za kiraia ,walinikuta nimekaa kwenye ukuta nikiwa na kijana mmoja,walinikamata na kunifunga pingu wakiwa wamenikandamizia chini ,walinipiga sana na kunivunja mikono yangu miwili''alisema Samweli

Akisimulia chanzo cha tukio  hilo alisema ,mfanyabishara bi Shamimu alienda katika kituo hicho cha polisi na kuwaeleza askari hao kuwa alikuwa akinidai shilingi 250,000 na kwamba sikuwa nimemlipa deni hilo.

''Ni kweli Shamimu alikuwa akinidai shilingi 250,000 ila nilisha mlipa shilingi laki moja na kubaki sh,150,000 ,hizo hela kuna msichana nilimdhamini alikuwa mfanyakazi wa duka lake aliyedai alimwibia ,ndipo mimi kwa kuwa nilikuwa na mahusiano na msichana huyo nilikubali kulilipa deni hilo''alisema Samweli

Alisema askari hao walimvamia na kumkaba kabali kisha askari mmoja alimfunga pingu na kuanza kumshambulia kwa kumpiga na rungu na chuma na walipoona wamepoteza fahamu baada ya kumvunja mikono walimkokota hadi kituo cha polisi na kuendelea kumpigasehemu zingine za mwili ikiwemo miguuni.

''baadae usiku wakiwa wamenifungia lokapu alikuja mkuu wa kituo na kuniangalia ,alikuta hali yangu ni mbaya na kuondoka bila kusema lolote''alisema.

Hata hivyo askari hao waliingiwa na woga kutokana na hali yake na kuamua kumchukua usiku huo wa manane na kumpeleka katika kituo cha afya kwa ajili ya matibabu.  

Alieleza kuwa kesho yake askari hao walimchukua na kumpeleka kituo cha polisi wilaya ya Monduli na kumwoka lokapu.Aliongeza kuwa mkuu wa upelelezi wa wilaya OC CID,aliyemtaja kwa jina moja la bw Abichi alimfuata akiwa lokapu na kumwambia kuwa anataka ampatie dhamana ila alitakiwa akibaliane na masharti ya dhamana .

''oc cid aliniambia kuwa nataka nikupatie dhamana ila kwenye maelezo yako unatakiwa ueleze kuwa ulikuwa unatoroka ulinzi halali wa polisi ukiwa na pingu ,na wakati ukikimbia ulianguaka na pingu zikakuvunja mikono yako ''alisema bw Shani.

Aliongeza kuwa hakukubaliana na kauli hiyo ndipo oc cid alipoamua kumrudisha lokapu ,ambapo alikaa kwa muda wa siku nne wakimbembeleza akubaliane na maelezo ya polisi .

Alisema kuwa aliamua kuwa na msimamo huo ,hadi tarehe 12 walipoamua kumfikisha mahakama ya wilaya ambapo alisomewa shtaka ,la kuvunja na kuiba na kujaribu kutoroka polisi akiwa na pingu ,suala ambalo ni uongo uliolenga kupoteza haki yake ya kulalamikia jeshi hilo.

Kamanda wa polisi mkoani hapa alipotafutwa alikiri kupata malalamiko ya mkazi huyo ,hata hivyo alieleza kuwa kwa sasa yupo likizo ila aliwasiliana na mkuu wa kituo cha polisi Monduli(OCD)ili kupata undani wa tukio hilo.

Kwa upande wa mfanyabiashara ,Shamimu alipotafutwa kupitia simu yake ya mkononi alikana kukodisha askari wa kumpiga na kumvunja mkono mlalamikaji ila alieleza kuwa yeye alienda kituoni hapo kupeleka malalamiko yake ,ndipo askari hao walipoamua kumfuata mtuhumiwa na kwamba kilichotokea huko yeye hafahamu.
habari picha kwa hisani ya libeneke la kaskazini blog
Posted by MROKI On Wednesday, February 25, 2015 No comments

BAADA

YA

KUIPANDISHA

MWADUI

FC

JAMHURI

KIWELO

'JULIO'

ATIMKIA

COAST

 Kocha Msaidizi wa Coastal Union,Jamhuri Kiwelu "Julio"kulia akisisitiza jambo mazoezini jana mara baada ya kuwasilia mkoani Tanga kuifundisha timu hiyo kushoto ni Kocha Mkuu James Nandwa ,Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Coastal Union,Albert Peter,Katibu Mkuu Coastal  Union,Kassim El Siagi na Meneja wa Coastal Union Akida Machai.
Kocha Msaidizi wa Coastal Union ,Jamhuri Kiwelu "Julio"akizungumza na viongozi wa Coastal Union mara baada ya kuwasili mazoezini jana.
Posted by MROKI On Wednesday, February 25, 2015 No comments

MIGODI

YA

DHAHABU

YA

GEITA,

BULYANHULU,

BUZWAGI

NA

NORTH

MARA

KUANZA

KULIPA

USHURU

WA

HUDUMA

KWA

KIWANGO

CHA

Posted by MROKI On Wednesday, February 25, 2015 No comments

RAIS

KIKWETE

APOKEA

MSAADA

WA

VITABU

VYA

MASOMO

YA

SAYANSI

KUTOKA

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe Paul Makonda baada ya kuwasili katika Shule ya Sekondari ya Mtakuja huko Kunduchi jijini Dar e salaam leo tayari kwa kukagua ujenzi wa maabara na pia kupokea na kugawa vitabu vya sayansi vilivyochapishwa  na Watu wa Marekani.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Mama Salma kikwete, Balozi wa Marekani nchini Mhe Mark Childress, Dkt Shukuru Kawambwa, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,na viongozi wengine wakiangalia jinsi somo la sayansi likifundishwa katika darasa la Kidatu cha pili Shule ya Sekondari ya Mtakuja huko Kunduchi jijini Dar e salaam ambako  pia alipokea na kugawa vitabu vya sayansi vilivyochapishwa  na Watu wa Marekani
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Mama Salma kikwete, Balozi wa Marekani nchini Mhe Mark Childress, Dkt Shukuru Kawambwa, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,na viongozi wengine wakisalimia wanafunzi katika   darasa la Kidatu cha pili Shule ya Sekondari ya Mtakuja huko Kunduchi jijini Dar e salaam ambako  pia alipokea na kugawa vitabu vya sayansi vilivyochapishwa na Watu wa Marekani
 Rais  Jakaya Mrisho Kikwete na Balozi wa Marekani nchini Mhe Mark Childress, wakiongea na mkandarasi wa maabara ya  Shule ya Sekondari ya Mtakuja huko Kunduchi jijini Dar e salaam ambako  pia alipokea na kugawa vitabu vya sayansi vilivyotolewa na Watu wa Marekani
 
Rais  Jakaya Mrisho Kikwete, Mama Salma Kikwete  na Balozi wa Marekani nchini Mhe Mark Childress wakiwa na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mtakuja huko Kunduchi jijini Dar e salaam wakiwa na vitabu vya sayansi vilivyochapishwa  na Watu wa Marekani
 Kikundi cha utamaduni cha jeshi la polisi kikitumbuiza katika sherehe ya kukabidhiwa vitabu vya sayansi vilivyotolewa na Watu wa Marekani

Posted by MROKI On Tuesday, February 24, 2015 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Blog Archive

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...