WANANCHI WAPINGA MWEKEZAJI MZAWA KUPORA ARDHI YA MALISHO YAO

Mkazi wa Kijiji cha Chemchem akilalama kwenye mkutano wa kumpinga mwekezaji

Wananchi wenye hasira kali wakichoma uzio wa muda.
Filbert Rweyemamu,Karatu
Wananchi wenye hasira  katika Kijiji cha Chemchem,Kata ya Rhotia wilayani Karatu wamevamia eneo la mwekezaji mzawa ,Samwel Kastuli na  kuharibu uzio wa muda na banda lililokua linalohifadhi vifaa vya ujenzi kwa kudai eneo hilo la zaidi ya heka 14  sio lake bali ni mali ya Kijiji kwaajili ya malisho ya mifugo.

Katika mkutano uliofanyika juzi kwenye eneo linalobishaniwa  na pande hizo zaidi ya wananchi 300 walikuwepo na kumwomba Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Magesa Mulongo na Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi,Profesa Anna Tibaijuka kuingilia kati mgogoro huo ili kuepusha madhara yanayoweza kutokea.

Mmoja wa wananchi hao,Hiiti Tlatlaa alisema hawatakubali eneo hilo lililopakana na Hifadhi ya taifa ya Ziwa Manyara lichukuliwe na mwekezaji yeyote wakati lilitengwa kwa shughuli za mifugo ya wanakijiji wote na bado kuna mahitaji ya ardhi kwaajili ya vijana wao.

Mwenyekiti wa kwanza wa Kijiji hicho kiliposajiliwa mwaka 1975,Mohe Bura na Martina Kastuli walidai mwekezaji amezungushia uzio kwenye  eneo la zaidi ya heka 100 wakati mwekezaji anadai ni eneo la heka 14,wanatambua wawekezaji wawili waliopewa ardhi kwa halali ambao ni Bulk Oil heka 80 na Zapata heka 7 na si vinginevyo.

“Kijiji chetu hakina uongozi wa tangu mwaka 2011 kwasababu ya viongozi walafi tuliowatimua madarakani ambao ni Mwenyekiti Tlatlaa Bura na Mtendaji wake wanaojitafutia maslahi yao bila kuwashilikisha wananchi tunaomba viongozi wetu wa ngazi ya juu watusaidie kuondoa kero hii,”alisema Bura

Kwa upande wake mwekezaji huyo,Samwel Kastuli alidai ameshachukua hatua za kisheria dhidi ya wananchi waliofanya uharibifu wa mali zake zikiwemo uporaji wa Saruji,Nondo na vifaa vingine kwaajili ya ujenzi wa hoteli ya kitalii.

Alisema ana hati halali za ununuzi wa eneo hilo kutoka kwa mkazi wa Kijiji hicho,Shauli Hhansa na amesikitishwa na uamuzi wa baadhi ya wananchi hao kwani mradi huo utakapokamilika utatoa ajira kwao.

Post a Comment

أحدث أقدم