![]() |
| Mjumbe wa Bodi ya Lake Eyasi Culture Tourism Programme,Ushoka Kidobadi |
Jamii za Wadzabe
na Watatoga kwenye bonde la Eyasi wanaoishi kwa kutegemea mapato
yanayotokana na utalii wa utamaduni kwenye maboma yao wamepinga mpango wa
halmashauri ya wilaya ya Karatu kuanzisha sheria itakayoipa mamlaka ya kuendesha
shughuli za utalii huo.
Wakizungumza kwenye mkutano wa wadau wa utalii wa
kiutamaduni juzi katika Kijiji cha Qangded Kata ya Baray walisema wanaipinga
sheria hiyo isisainiwe na Waziri Mkuu,Mizengo Pinda kwasababu itaharibu kabisa
utalii wao ambao wanautegemea kama njia kuu ya mapato na kudumisha mila na
desturi zao.
Mwenyekiti wa muda wa Lake Eyasi Cultural Tourism
Programe,Issa Ngimba alisema Programu ya Utalii wa kiutamaduni ilipata baraka na
inaratibiwa na bodi ya Utalii nchini(TTB)na utaratibu wa sasa kila gari la
watalii linalipa Sh 30,000 wakati halmashauri ya wilaya inapata Sh.7,500 na pesa
nyingine zinaenda kwenye ofisi za vijiji vitatu ambako utalii unafanyika.
Sehemu ya tangazo hilo inasema, Ada za utalii zitatozwa
katika katika maeneo ya utalii zitakua ni moja ya chanzo cha mapato cha
halmashauri pamoja na maendeleo ya kijiji tu na si kwaajili ya makundi maalum
kama Tatoga,Wahunzi na Hadzabe na baada ya kukusanywa asilimia 20 itarudishwa
kwenye kijiji kilichohusika na utalii huo.
Katika viwango vya halmashauri inapendekeza kila mtalii
wa nje ya nchi atalipa Sh.15,000 wakati awali walikua hawalipi bali gari tu ndio
lilikua linatozwa huku watalii wanafunzi wa nje watatozwa Sh.7,500
na halmashauri ndio ita waajiri waongoza watalii jambo wanalolipinga.
Hata hivyo mmoja wa wajumbe wa bodi ya Lake Eyasi
Cultural Tourism Programe,Ushoka Kidobadi alisema hawaamini kama halmashauri
itarudisha asilimia 20 kwao kwani tangu halmashauri imeanza kutoza dola tano
haijawahi kurejesha kwa wananchi kiasi chochote.
“Hatuko tayari kuunga mkono halmashauri yetu katika
hili jambo,sisi tunatumia muda mwingi kukaa kwenye maboma yetu kuelimisha
watalii halafu wao wanataka kubinafsisha utamaduni wetu kwa kisingizio cha
kuongeza mapato ambayo hata hayatusaidii wananchi.”alisema
Ginyanyi Gisulu alidai iwapo halmashauri itang’ang’ania
uamuzi wake,wao hawatatoa ushirikiano kwa waongoza utalii na hawatawaruhusu
kufika kwenye maboma yao kwani kiwango kipya ambacho halmashauri inakusudia
kutoza kitapunguza watalii na hawataweza kununua zawadi za kiasili kwenye maboma
yao.
Alisema jamii ya wadzabe ambao hutegemea uwindaji na
kuchimba mizizi,watalii ndio chanzo cha mapato yao yanayowasaidia kulipia
gharama za matibabu,elimu na kununulia chakula hivyo kuona mpamgo huo kama wenye
lengo la kurudisha nyuma maendeleo yao.
![]() |
| Mwanzilishi wa Utalii wa Utamaduni kwenye bonde la Lake Eyasi wilayani Karatu,mkoa wa Arusha,Momaya |
![]() |
| Wanawake wa jamii wa Tatoga wakifatilia mkutano |
![]() |
| Wajumbe kutoka jamiiya Kihadzabe na Tatoga wakiwa kwenye mkutano |





إرسال تعليق