Pages

May 7, 2013

CCM YAIBWAGA CHADEMA SUMBAWANGA


Aeshi Hilary.YamseboAliekuwa mgombea wa CHADEMA, Mwalimu Norbet Yamsebo akiwa na furaha mara baada ya kuibuka mshindi
Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga kutengua matokeo ya ubunge wa jimbo la Sumbawanga mjini yaliyompa ushindi mgombea wake Aeshi Hilal. 
MAHAKAMA ya Rufani Tanzania imerejesha ubunge wa Sumbawanga Mjini kwa Aeshi Hilary (CCM) uliotenguliwa na Mahakama Kuu kanda ya Sumbawanga kwenye kesi ya kupinga uhalali wa matokeo yaliyompa ushindi mbunge huyo.

Hukumu ya rufani hiyo ilisomwa Dar es Salaam jana na Naibu Msajili wa Mahakama Zahara Maruma na kueleza kuwa sababu zilizotumika kutengua ubunge huo hazikuthibitika.

Aeshi alichaguliwa kuwa mbunge wa Sumbawanga mjini wakati wa uchaguzi wa mwaka 2010 baada ya kuwashinda wagombea wengine akiwemo Norbet Yamsebo (CHADEMA) ambaye alifungua kesi kupinga matokeo hayo.

Naibu msajili huyo alizitaja sababu hizo kuwa ni vurugu wakati wa kampeni zilizosababisha Yamsebo kushindwa kufanya mikutano yake na madai ya rushwa iliyotolewa na mawakala wa Aeshi kwenye shule ya msingi Kantalamba Mazoezini.

Akisoma hukumu hiyo, Naibu Msajili alisema kulikuwa na mkanganyiko kwenye ushahidi uliotolewa Mahakama Kuu ambapo mashahidi walishindwa kuonyesha namna vurugu hizo zilivyoathiri matokeo ya uchaguzi.

Kuhusu madai ya rushwa Mahakama ya Rufani imetilia shaka ushahidi uliotolewa na mtu mmoja aliyedai kwamba aliwaona mawakala wa Aeshi wakitoa fedha huku akishindwa kuthibitisha madai hayo.

Awali Aeshi alikata rufani kupinga hukumu ya kutenguliwa kwa ubunge wake iliyosomwa Aprili 30, 2013 na aliyekua Jaji wa Mahakama Kuu kanda ya Sumba

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...