Serikali inaendelea na utekelezaji wa mkakati wake wa kuhakikisha Tanzania inakuwa kitovu cha uzalishaji wa bidhaa zinazotumika migodini na kupunguza uagizaji wa bidhaa hizo kutoka nje ya nchi.
Hayo yamesemwa leo tarehe 13 Aprili, 2025 na Waziri wa Madini, Mh.Anthony Mavunde (Mb) alipotembelea na kuzindua kiwanda cha uzalishaji wa baruti na vilipuzi cha Solar Nitrochemicals Limited kilichopo Wilayani Kisarawe.
"Mh. Rais wetu Dkt. Samia S. Hassan anafanya kazi kubwa ya kufungua fursa na kuweka mazingira mazuri yanayovutia uwekezaji nchini. Matokeo ya kazi hiyo ni pamoja na ujenzi wa kiwanda hiki cha kuzalisha bidhaa hizi ambazo ni muhimu sana kwenye uchimbaji wa madini.
"Kama Serikali, tutaendelea kuwalinda wawekezaji wetu na kuwawekea mazingira wezeshi ili waendelee kuleta uwekezaji wenye tija utakaosaidia pia kuongeza mapato ya Serikali na ajira kwa watanzania.
Matumizi ya baruti nchini ni tani 26,000 na vilipuzi pisi milioni 10 kwa mwaka, hivyo ujio wa kiwanda hichi kitakachozalisha tani 22,000 za baruti na vilipuzi pisi milioni 15 utasaidia kukidhi mahitaji ya ndani ya nchi na kuuza katika nchi zinazotuzunguka.
Uzalishaji wa baruti na vilipuzi ndani ya nchi utasaidia kupunguza gharama ya bidhaa hiyo kwa wachimbaji, ajira kwa wananchi na kuongeza ujuzi na elimu kwa watanzania.
Awali, Mkurugenzi Mkazi wa Kampuni ya Solar Nitrochemicals Limited, Bw. Kishor Bhomale alieleza kuwa ujenzi wa kiwanda hicho umegarimu Dola za Kimarekani Milioni 8 Sawa na Shilingi za Kitanzania bilioni 19 na wamelenga kuzalisha kwa ajili ya soko la ndani na nje ya nchi.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Mh. Petro Magoti alieleza kuwa uwepo wa kiwanda hicho utachochea ukuaji wa kiuchumi wa Kisarawe na pia wametenga eneo kubwa kwa ajili ya viwanda na kwamba wapo tayari kupokea wawekezaji katika ujenzi wa viwanda vya kuzalisha bidhaa mbalimbali.
On Monday, April 14, 2025No comments

Katika hafla hiyo hiyo, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muunganowa Tanzania, ametunukiwa tuzo ya Heshima ya Kipekee kwa Uongozi wa Kiwango cha Juu Barani Afrika (Imperial Honour for African Iconic Global Leadership of the Year).
Hili ni tukio la kihistoria kwa Tanzania ambapowanawake viongozi wawili wametambuliwa kwa heshima za juu kabisa katika bara la Afrika siku moja. Huu ni ushahidi wa nguvu, ushawishi, na msukumo mkubwa wa wanawake wa Kitanzaniakatika jukwaa la kimataifa.
Tuzo ya Tully ni matokeo ya juhudi zake kubwakatika kuwawezesha wanawake na vijana kupitia programu jumuishi na bunifu za kifedha. Uongoziwake ndani ya CRDB Bank Foundation umebadilimaisha ya maelfu ya Watanzania, hususanwajasiriamali vijana na wanawake kupitia programu ya iMbeju, ambapo ndani ya mwaka mmoja tokeakuanzishwa kwake imefikia zaidi ya wanawake na vijana 800,000. Programu ya iMbeju inatoa mafunzo ya ujasiriamali, ushauri, elimu ya fedha, na mitaji wezeshi.
Tully ana uzoefu wa zaidi ya miaka 20 katika sektaya benki, ambapo amehusika katika kubuni bidhaa na huduma bunifu zilizochangia kupanua wigo wa ujumuishi wa kifedha nchini. Kupitia CRDB Bank Foundation, anaendelea kuwa chachu ya matumainina mabadiliko chanya katika jamii.
Tuzo hii imekuja katika kipindi cha kipekee ikiwa ni miaka 30 tangu Azimio la Beijing, mpango muhimuwa kihistoria wa kuendeleza haki na usawa wa wanawake duniani. Pia, tuzo hii imekuja wakatiBenki ya CRDB ikisherehekea miaka 30 tangukuanzishwa kwake, ikiwa ni taasisi ya kifedha inayozidi kuonesha dhamira ya dhati katika kuwawezesha wanawake.
Wakati dunia inatafakari mafanikio ya miaka 30 ya harakati za usawa wa kijinsia tangu Beijing, na wakati Benki ya CRDB ikisherehekea miongo mitatuya huduma kwa Watanzania, tuzo ya Tully inakuwaalama hai ya mafanikio haya. Kazi yake inaakisimalengo ya Azimio la Beijing katika kuondoavikwazo, kutoa fursa kwa wanawake, na kuinuajamii.
Tuzo hii pia inaipa Benki ya CRDB nafasi ya pekeeya kuwa miongoni mwa taasisi za kifedha barani Afrika ambazo haziegemei tu upande wa ujumuishwaji wa kifedha, bali pia zinakuwa mstariwa mbele katika kufanikisha usawa wa kijinsia na maendeleo endelevu. Aidha, inadhihirisha falsafa ya kipekee ya CRDB Bank Foundation katika kutumiahuduma za kifedha kuchohea maendeleo ya kijamii, huku ikithibitisha kuwa benki inaweza kuwa na lengo la zaidi ya kutafuta faida, na kuwa chombo cha kusukuma mabadiliko ya kiuchumi na kijamii.
Katika tuzo hii Tully ameibuka mshindi dhidi ya viongozi wengine wanawake mashuhuri barani Afrika ikiwamo Odunayo Sanya, Mkurugenzi Mkuuwa MTN Foundation, Balo Atta, Afisa Mtendaji Mkuu wa UBA Foundation), Osayi Alile Afisa Mtendaji Mkuu wa Aspire Coronation Trust Foundation), Somachi Chris-Asoluka, Afisa Mtendaji Mkuu wa Tony Elumelu Foundation, na Claire Akamanzi, Afisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Maendeleo Rwanda.
Ushindi wa Tully ni uthibitisho muhimu kuwawanawake wana nafasi muhimu ya kubadili maisha na kuchochea maendeleo katika jamii na Taifa.
Post a Comment