Arusha.Watu wasiojulikana wameingilia mawasiliano ya simu za
mkononi za Mkuu wa wilaya ya Arusha,Fadhili Nkurlu na kuwatumia ujumbe mfupi
watu walio karibu nae kwa kuwaomba fedha kati ya Sh 1 milioni hadi 2 milioni .
Akizungumza
na waandishi wa habari jana ofisini kwake,Nkurlu alisema watu hao
walikata kwanza mawasiliano kwenye simu zake mbili na baadaye kusajili
upya laini zenye majina yake kuanzia saa 10 jioni hadi jana asubuhi na
katika kipindi hicho kifupi walikua wameshajipatia kiasi cha Sh 10
milioni.
"Mwanzoni
nilidhani kuna shida ya mawasiliano kwasababu hakuna simu iliyokua
inatoka wala kuingia,ilipofika saa tatu usiku nilijaribu kutumia simu
nyingine mbali na mitandao ya Voda na airtel ninazotumia mara kwa mara
ikafanya kazi na kumtaarifu mke wangu aliyeniambia simu zangu zilikua
hazipatikani na baadhi yao walinijulisha kuwa wametumiwa ujumbe mfupi wa
kuomba msaada wa fedha ,"alisema Nkurlu
Alisema
baada ya kukutwa na hali hiyo anaamini kuna mawasiliano kati ya
wahalifu wa mitandao na baadhi ya wafanyakazi kwenye makampuni za simu
wasio waaminifu wanaotoa taarifa za undani za watu ambao anawasiliana
nao mara kwa mara na namna walivyoweza kusajili upya namba bila
kitambulisho.
Aliwaasa
wananchi kuwa makini kwa kutokutoa fedha kwa wanaowatumia ujumbe mfupi
hadi wazungumze nao na kujiridhisha kama ni kweli waliowatumia ujumbe ni
watu halisi na kuepuka utapeli ulioshamiri nchini kupitia njia ya
mitandao.
"Nalaani
kitendo hiki kwa nguvu zote kwasababu hakiwezi kufanikiwa bila
ushirikiano na wafanyakazi wa makampuni ya simu,sasa najiuliza fedha
zetu ziko salama kiasi gani kwenye mitandao ya simu au wale wanaotumia
huduma za benki kwa kutumia simu,"alihoji
Aliitaka
mamlaka ya mawasiliano nchini (TCRA)kufanya uchunguzi wa kina kwenye
makampuni ya simu ili kujiridhisha kama wafanyakazi hawashirikiani na
wahalifu wa mitandao na kuweka sheria kali ya namna ya kukabiliana nao.
Baadhi
ya waliotumiwa ujumbe wa kutaka fedha ni Mkuu wa wilaya ya
Ngorongoro,Hashim Mgandilwa aliyeombwa Sh 2 milioni na Msaidizi wa Mkuu
wa Mkoa wa Arusha,Yotham Ndembeka aliyeombwa Sh 1 milioni.
Ndembeka
alisema baada ya kupata ujumbe huo alimwambia hakua na kiasi hicho
lakini wahalifu hao walitaka atume kiasi chochote kwani kingerudishwa
jana asubuhi kutokana na dharula aliyokua nayo.
"Nilimwambia
Mkuu wa wilaya ninaenda nyumbani kwake kumuona uso kwa uso lakini
alikataa akidai yuko kwenye kikao cha dharula,kila nilipojaribu kumpigia
hakua anapokea simu nikafahamu hakua mtu sahihi ninayemfahamu,"alisema
Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha,Liberatus Sabas alisema hakua amepata taarifa rasmi ya tukio hilo ofisini kwake.
No comments:
Post a Comment