Pages

March 19, 2018

KAMATI YA BUNGE YATEMBELEA MAPORI YA AKIBA YA BIHARAMULO, BURIGI, KIMISI (BBK) MKOANI KAGERA

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Nape Nnauye akiwaongoza baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo kushuhudia maporomoko ya maji ya Rusumo yaliyopo wilayani Ngara ambapo moja ya vyanzo vyake vikubwa vya maji vimeanzia katika Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi na Kimisi (BBK) wakati Kamati hiyo ilipofanya ziara mwishoni mwa wiki mkoani wa Kagera.
Wajumbe wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakipewa maelezo kuhusu mipaka ya Pori la Akiba ya Biharamulo kutoka ziwa Victoria katika kituo cha Katete kutoka kwa Meneja wa Mapori ya Biharamulo, Burigi, Kimisi (BBK), Bw. Bigilamungu Kagoma (wa kwanza kushoto) wakati Kamati hiyo ilipotembelea mapori yaliyopo mkoani Kagera mwishoni mwa wiki
Meneja wa Mapori ya Biharamulo, Burigi, Kimisi (BBK), Bw. Bigilamungu Kagoma (wa kwanza kushoto) akiwaonesha Wajumbe wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii katika ramani mahali ambako Pori la Akiba la Burigi lilipoanzia wakati Kamati hiyo ilipofanya ziara katika Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi, Kimisi (BBK), yaliyopo mkoani Kagera hayo mwishoni mwa wiki mkoani Kagera
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Nape Nnauye akiwazungumza na baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo mara baada ya kujionea Pori la Akiba la Burigi katika wilaya ya Karagwe ambayo ni moja ya kati avyanzo vyake vikubwa vya maji ambavyo vimeanzia katika Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi na Kimisi (BBK) wakati kamati hiyo ilipofanya ziara mwishoni mwa wiki mkoani wa Kagera.Wajumbe wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakiangalia hema ambalo askari wanyamapori hulitumia kumpumzika wakiwa katika Mapori wakati wanapofanya doria za kuwabaini majangili.Meneja wa mpaka katika Tanzania na Rwanda ambaye pia ni Afisa Mwandamizi wa Forodha, Polycarp Lashau akiwaongoza Wajumbe wa kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kushuhudia maporomoko ya maji ya Rusumo yaliyopo wilayani Ngara ambapo moja ya vyanzo vyake vikubwa vya maji vimeanzia katika Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi na Kimisi (BBK) wakati Kamati hiyo ilipofanya ziara mwishoni mwa wiki mkoani wa KageraWajumbe wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakipewa maelezo kuhusiana na mali mbalimbali za watuhumiwa wa ujangili zikiwemo baiskeli na pikipiki zilizokamatwa katika kituo cha Katete kwenye Pori la Akiba ya Biharamulo kutoka kwa Meneja wa Mapori ya Biharamulo, Burigi, Kimisi (BBK), Bw. Bigilamungu Kagoma (wa kwanza kushoto) wakati Kamati hiyo ilipotembelea mapori yaliyopo mkoani Kagera hayo mwishoni mwa wiki
(PICHA ZOTE NA LUSUNGU HELELA-MNRT)

Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii ambayo ipo mkoani Kagera imeridhishwa na utendaji kazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) baada ya kutembelea Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi na Kimisi (BBK) kuangalia kazi za uhifadhi zinazofanywa ambapo wameipongeza TAWA kwa kitendo cha kurudisha hali ya mapori hayo ikiwemo kurejea kwa wanyamapori na uoto wa asili ambapo awali mapori hayo yalikuwa yameharibiwa kwa kasi kutokana na makundi ya mifugo kufanya malisho katika maeneo hayo.
Katika ziara hiyo,iliyoanzia katika Wilaya ya Biharamulo, Wajumbe wa Kamati hiyo waliweza kushuhudia eneo la Pori hilo lilipoanzia katika ziwa Victoria na baadaye kushuhudia Pori la Burigi lililopo katika wilaya za Karagwe na Biharamulo na badaye Pori la Kimisi ambalo lipo katika wilaya mbili za Karagwe na Ngara.
Hata hivyo,Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Nape Nnauye aliridhishwa na masuala ya uendeshaji wa mapori hayo huku akiahidi kuyasaidia mapori hayo kwa kuishauri serikali iweze kuwekeza miundombinu ili kukuza utalii katika ukanda wa ziwa Victoria
‘’Tunatambua kuwa TAWA ni changa haijaanzishwa muda mrefu lakini ndani ya kipindi kifupi imeweza kufanya mambo mazuri katika kulinda Maliasili zetu , Sisi kamati tumeridhisha na utendaji wake’’ alisema Mwenyekiti
Kutokana na utendaji kazi wa Mamlaka hiyo , ‘Mwenyekiti wa Kamati hiyo iliahidi kuwa watalishauri na pamoja na kuishawishi Serikali iweze kuongeza pesa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2018/2019 ili iweze kutimiza wajibu yake.
Kwa upande wake, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla aliielezea kamati hiyo kuwa TAWA ipo mbioni kubadili mfumo wake katika mapori hayo ambapo badala ya kuendelea kufanya shughuli za uwindaji wa kitalii pekee wamepanga kuanzisha utalii wa picha ili kufungua fursa za kiuchumi katika ukanda huo.
Aidha, Waziri Kigwangalla alisema kuwa kutokana na Mapori hayo kurejea katika uasilia wake baada kuharibiwa kwa kiasi kikubwa na uvamizi wa mifugo hali iliyopelekea hadi wanyamapori kuhama, Wizara inafanya utafiti ili kuongeza baadhi ya wanyama katika Mapori hayo ili kuweza kuwavutia watalii zaidi kutembelea maeneo hayo.
Aliongeza kuwa, mapori hayo yana sifa ya pekee za kumvutia mtalii yeyote aweze kutembelea katika maeneo hayo huku ukitaja wanyamapori wanne wakubwa kuwa wanapatika katika mapori hayo isipokuwa faru pekee.
Awali kamati hiyo ilipokea taarifa kutoka kwa Wenyeviti wa Kamati za ulinzi na usalama za wilaya ambapo miongoni mwa mambo yaliyojitokeza uvamizi wa maeneo ya mapori ya akiba kwa kuanzisha shughuli za kilimo pamoja na kulisha mifugo ndani ya hifadhi.
Naye, Mtendaji Mkuu wa TAWA, James Wakibara alisema moja ya mikakati ya TAWA ni kubadilisha aina ya biashara kwa kuanza kuchanganya ambapo TAWA itaendesha biashara ya uwindaji wa vitalu pamoja na utalii wa picha katika mapori hayo kwa lengo la kuiongezea serikali mapato
Alisema Serikali ipo katika mchakato wa kuboresha miundombinu kwa kuanza na barabara ndani ya mapori hayo ili kuweza kuwavutia wawekezaji kujenga hoteli mbalimbali ambazo watalii watazitumia kwa ajili ya kupumzika.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...