Pages

December 14, 2017

SERIKALI YAWEKA MIKAKATI YA KUWAONDOA VIJANA KATIKA MAZINGIRA HATARISHI WASHIRIKI SHUGHULI ZA KIUCHUMI

Na EmanuelMadafa,Mbeya ,JamiiMojaBlog
Serikali inayo wajibu wa kuhakikisha kuwa inawaondoa vijana kwenye mazingira hatarishi na kuhimiza ushiriki wao kwenye shughuli za kijamii na kiuchumi ili kuleta maendeleo katika ngazi zote.
 
Imeelezwa kuwa takribani asilimia 56 ya nguvu kazi ya Taifa ni vijana wenye umri  kati ya miaka 15 hadi 35  kwa mujibu wa ripoti ya nguvu kazi ya mwaka 2014 .
 
Akizungumza jijini Mbeya wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya stadi za maisha kwa wawezeshaji kanda ya magharibi,Mkurugenzi wa maendeleo ya vijana Ofisi ya Waziri Mkuu ,kazi,Vijana ,ajira na wenye ulemavu Ndugu Jemsi Kujusi amesema serikali mara baada ya kubaini hali hilo iliamua kutengeneza  viwango vya ufundishaji wa stadi za maisha kwa vijana nje ya shule kwa kuandaa muongozo sanifu.
 
Amesema muongozo huo ulinzinduliwa mwaka 2011 na baada ya hapo iliendelea na jitihada za kuhakikisha kuwa kunakuwa na wawezeshaji wa kitaifa ambao jukumu lao linakuwa ni kutoa mafunzo kwa waelimishaji rika katika mikoa yao ili kuwafikia vijana wengi zaidi kwa ngazi zote.
 
Mkurugenzi huyo amesema kazi ya kuwaanda vijana kuwa wawezeshaji kitaifa ilianza Kanda ya Ziwa mwaka 2015  ambapo serikali iliendelea na jitihada za kuendeshav mafunzo kwa wawezeshaji kitaifa kutoka mikoa ya kanda ya kati ,Pwani na mashariki.
 
Amesema hadi Agosti 2017 jumla ya wawezeshaji kitaifa 60 walikuwa wamefikiwa ambapo lengo la serikali ni kuwa na wawezeshaji 78 kwa nchi nzima .
 
Mkurugenzi huyo amewataka washiriki wa mafunzo hayo kwa kanda ya magharibi ambo ni ,Ruvuma,Kigoma,Songwe,Mbeya,Katavi kuhakikisha kuwa wanatambua kuwa wanajukumu kubwa kwani serikali kupitia wao inataka kuona vijana wakishiriki kwenye shughuli mbalimbali za kiuchumi na kuachana tabia za kukaa vijiweni.

Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana ,Ajira na Wenye Ulemavu Ndugu Jemsi Kujusi akifungua mafunzo ya stadi za maisha kwa wawezeshaji kitaifa kanda ya Magharibi katika ukumbi wa Hospital ya Rufaa Mbeya Desemba 13 .

Washiriki wa Mafunzo  ya stadi za maisha kwa wawezeshaji kitaifa kanda ya Magharibi  wakisikiliza kwa makini hotuba ya Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana ,Ajira na Wenye Ulemavu  (hayupo Pichani )Ndugu Jemsi Kujusi  katika ukumbi wa Hospital ya Rufaa Mbeya Desemba 13 .

Mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya katika  mafunzo hayo Ndugu George Mbigima akizunngumza katika mafunzo hayo

Washiriki wakifuatilia kwa makini mafunzo.

Afisa Maendeleo ya jamii jiji la Mbeya ambaye ni Mwenyekiti wa Mafunzo  ya Stadi za Maisha kwa wawezeshaji kitaifa Kanda ya Magharibi Mkoa wa Mbeya  Ndugu Baraka  Mronga akitoa neno la shukrani kwa mgeni rasmi katika mafunzo hayo.;

Washiriki wa Mafunzo  ya stadi za maisha kwa wawezeshaji kitaifa kanda ya Magharibi katika picha ya pamoja na Mgeni rasmi
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana ,Ajira na Wenye Ulemavu Ndugu Jemsi Kujusi Ukumbi wa Hospital ya Rufaa Mbeya.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana ,Ajira na Wenye Ulemavu Ndugu Jemsi Kujusi akifungua mafunzo ya stadi za maisha kwa wawezeshaji kitaifa kanda ya Magharibi katika ukumbi wa Hospital ya Rufaa Mbeya Desemba 13 .

Washiriki wa Mafunzo  ya stadi za maisha kwa wawezeshaji kitaifa kanda ya Magharibi  wakisikiliza kwa makini hotuba ya Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana ,Ajira na Wenye Ulemavu  (hayupo Pichani )Ndugu Jemsi Kujusi  katika ukumbi wa Hospital ya Rufaa Mbeya Desemba 13 .

Mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya katika  mafunzo hayo Ndugu George Mbigima akizunngumza katika mafunzo hayo

Washiriki wakifuatilia kwa makini mafunzo.

Afisa Maendeleo ya jamii jiji la Mbeya ambaye ni Mwenyekiti wa Mafunzo  ya Stadi za Maisha kwa wawezeshaji kitaifa Kanda ya Magharibi Mkoa wa Mbeya  Ndugu Baraka  Mronga akitoa neno la shukrani kwa mgeni rasmi katika mafunzo hayo.;

Washiriki wa Mafunzo  ya stadi za maisha kwa wawezeshaji kitaifa kanda ya Magharibi katika picha ya pamoja na Mgeni rasmi
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana ,Ajira na Wenye Ulemavu Ndugu Jemsi Kujusi Ukumbi wa Hospital ya Rufaa Mbeya.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...