SERIKALI YAJIDHATITI KULINDA HAKI ZA WATOTO NCHINI

Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Dk Hamisi Kigwangalla(kulia)akiagana na Afisa Mtendaji Mkuu wa taasisi REPSSI Afrika ,Noreen Huni(katikati) mara baada ya kufungua mkutano wa siku tatu wa taasisi hiyo inayojihusisha na kutoa ushauri wa kisaikolojia kwa watoto katika nchi za Kusini na Mashariki mwa Afrika  jijini Arusha,kushoto ni Mkurugenzi wa REPSSI nchini,Edwick Maphalala na wa pili kulia ni Mjumbe wa Bodi REPSSI Afrika,Jeanne Ndyetabura.Picha na Filbert Rweyemamu


Wajumbe wa mkutano wa ushuri wa kisaikolojia kwa watoto wakifatilia mada katika mkutano wa siku tatu jijni Arusha  ulioandaliwa na taasisi ya REPSSI.


Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Dk Hamisi Kigwangalla akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufungua mkutano huo.  

Filbert Rweyemamu,Arusha.
Serikali imesema licha ya jitihada inazofanya kwa kushirikiana na wadau mbalimbali bado zipo changamoto zinazowakabili watoto nchini hivyo imeanda mpango wa kitaifa utakaotumika kuwalinda watoto dhidi ya vitendo vya ukatili.

Hayo yamesemwa  na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Hamisi Kigwangalla wakati akifungua mkutano wa siku tatu ulioandaliwa na taasisi ya REPSSI inayojihusisha na ushauri wa kisaikolojia na malezi kwa watoto katika nchi za Kusini na Mashariki mwa Afrika.

Alisema kupitia taasisi zake iliandaa mikakati nane ambayo hadi mwaka walikubaliana kuinganisha mikakati hiyo ili kupata mpango mmoja wa kitaifa ambao unazuia vitendo vya ukatili kwa wanawake na watoto.

"Katika mpango huo tunaeleza majukumu ya kila taasisi za serikali,binafsi na taasisi za kimataifa zinazojihusisha na kupiga vita vitendo vya ukatili dhidi ya watoto ndio utakaotumika katika kipindi cha mwaka 2017 hadi 2022 ili tumbunguze vitendo hivi kwa asilimia 50,"alisema Kingwangalla

Aliongeza kuwa mpango huo umeongeza adhabu kwa watakaobainika kuwafanyia watoto vitendo vya ukatili na umekusudia kujenga mahusiano ya karibu na taasisi zote ili kurahisha kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wanaopatikana na makosa hayo.

Dk Kigwangalla alisema hapa nchi takwimu za mwaka 2009 za utafiti zinaonesha kati ya watoto watatu wa kike mmoja amefanyiwa vitendo vya ukatili wa ngono akiwa chini ya miaka 18 wakati kati ya watoto saba mmoja amefanyiwa ukatili wa kijinsia.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika(EAC)Balozi Liberat Mfumukeko alisema watoto na vijana katika nchi za jumuiya wanafikia asilimia 50 lakiniwanakabiliwa na migogoro  ya kivita,Ukimwi,ukutili wa kingono,matendo ya udhalilishaji,ukahaba katika umri mdogo na umasikini.

Alisema kama jumuiya imeweka utaratibu wa kuwalinda watoto kwa kuanzisha baraza la kanda linalojihusisha na jinsia,vijana,watoto,maendeleo ya jamii na ulinzi kwa lengo la kuhakikisha nchi wanachama wanazingatia mpango pamoja ile iliyo katika nchi zao.

Naye Mkurugenzi wa REPSSI hapa nchini,Edwick Maphalala amesema jamii nzima inao wajibu wa kujenga mazingira mazuri ya kuhakikisha haki za watoto zinalindwa na inapotokea watoto wameathirika na matatizo ya mapigano wanatakiwa kupewa ushauri wa kisaikolojia.

Mkutano huo ni saba kufanyika tangu kuanzishwa  kwa taasisi hiyo miaka 15 iliyopita na imeweza kuwakutanisha watoto kutoka mataifa 31.

Post a Comment

Previous Post Next Post