TSSA YATEMBELEA KIWANDA CHA NYAMA MJINI SHINYANGA

Wakuu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii nchini kupitia Jumuiya yake ya TSSA (Tanzania Social Security Association), wakiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Adam Mayingu (wa pili kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa GEPF, Daud Msangi (wa pili kulia) wakiwa katika ziara ya kutembelea kiwanda cha nyama kilichopo mjini Shinyanga jana ambacho hakikuwahi kufanya uzalishaji tangu kibinafisishwe. Ziara hiyo ya viongozi hao ilikuwa ni kwa ajili ya kuona hali halisi ya kiwanda hicho ambacho kwa sasa kipo chini ya mikono ya Serikali, Mifuko hiyo kwa pamoja kupitia umoja wao wa TSSA wamedhamiria kuwekeza katika kwa pamoja katika sekta ya ngozi, nyama na nguo.
Wakuu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii nchini kupitia Jumuiya yake ya TSSA (Tanzania Social Security Association) wakipatiwa maelezo wakati walipotembelea kiwanda cha nyama kilichopo mjini Shinyanga, ambacho hakikuwahi kufanya uzalishaji tangu kibinafisishwe. 
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa GEPF, Daud Msangi akisaini kitabu wakati walipotembelea kiwanda cha nyama kilichopo mjini Shinyanga, ambacho hakikuwahi kufanya uzalishaji tangu kibinafisishwe. Kulia ni Katibu Mkuu wa Jumuiya ya TSSA, Meshack Bandawe.
Wakikiangalia maeneo mbalimbali ya usindikaji Nyama.
Wakuu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii nchini kupitia Jumuiya yake ya TSSA (Tanzania Social Security Association) wakiendelea na ziara yao katika kiwanda cha nyama kilichopo mjini Shinyanga.
Sehemu ya Majengo ya kiwanda hicho.

Post a Comment

Previous Post Next Post