WAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa amewataka Wahandisi Washauri nchini kutotumia
vibaya vyeo na dhamana walizonazo kwa kuwalazimisha wakandarasi kununua
bidhaa sehemu wanazotaka wao na badala yake wawashauri kununua bidhaa
bora.
Pia
amewataka watendaji wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Wakurugenzi wa
Halmashauri na Majiji nchini pamoja na Wahandisi Washauri kutumia
mabomba yanayozalishwa na viwanda vya ndani kwa kuwa yanakidhi viwango
vya ubora.
Waziri
Mkuu ametoa agizo hilo leo (Jumamosi, Desemba 3, 2016) wakati wa
uzindizi wa kiwanda cha kutengeneza bidhaa za plastiki cha Lodhia, akiwa
katika siku ya pili ya ziara yake ya kikazi mkoani Arusha.
“Serikali
inalenga kumaliza tatizo la ajira hasa kwa vijana na Serikali pekee
haiwezi kuwaajiri watu wote. Viwanda pekee ndivyo vyenye uwezo wa
kuzalisha ajira nyingi. Jukumu letu ni kuviunga mkono,” amesema.
Amesema
haoni sababu ya halmashauri na wakandarasi kununua mabomba kutoka nje
ya Arusha au nje ya nchi wakati bidhaa hizo zinazalishwa na wawekezaji
ndani ya mkoa huo na zinakidhi viwango vya ubora.
Hata
hivto Waziri Mkuu amewataka watumishi wa kiwanda hicho kufanya kazi kwa
weledi na uaminifu mkubwa ili kukiwezesha kuzalisha bidhaa nyingi zaidi
na hatimaye kuongeza ajira.
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda hicho, Sailesh Pandit
amesema moja ya changamoto kubwa inayowakabili kiwandani hapo ni
kushindwa kuuza bidhaa wanazozalisha katika miradi mikubwa ya maji
iliyotekelezwa Mkoani Arusha.
Amesema
“licha ya kuwa na viwango vya ubora vilivyothibitishwa na Shirika la
Viwango Tanzania (TBS) na ISO tunashindwa kuuza kutokana na hujuma
tunazofanyiwa na baadhi ya wahandisi wa Halmashauri na washauri elekezi
wa miradi ya maji mkoani hapa,”.
Mkurugenzi
huyo alisema "Mheshimiwa Waziri Mkuu mara kadhaa wakandarasi wamezuiwa
kununua mabomba ya maji kutoka kwenye kampuni yetu na badala
yake hulazimishwa kununua mabomba kutoka nje ya Mkoa wa Arusha na
kuisababishia serikali gharama zisizo za lazima "
Amesema
kampuni hiyo imetoa ajira rasmi kwa Watanzania 1,300 huku wengine zaidi
ya 500 wakinufaika kutokana na ushiriki wao katika utoaji wa huduma
kiwandani hapo. Kiwanda kinalipa wastani wa sh. bilioni 20 kwa mwaka
kama kodi na tozo mbalimbali.
Baada
ya kutoka kiwandani hapo Waziri Mkuu alitembelea kiwanda cha kutengeneza
bodi za magari cha Hanspaul ambapo amewataka Wakurugenzi wa halmashauro
zote nchini wanaohitaji magari ya kuzolea taka kwenda kununua katika
kiwanda hicho.
“Tumekua
tunanunua magari ya kuzolea taka kwa gharama kubwa ambayo ni kati ya
sh. milioni 300 hadi sh. milioni 400 kutoka nje ya nchi wakati magari
hayo yanapatikana Tanzania tena mkoani Arusha kwa sh. milioni 200,”
amesema.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
JUMAMOSI, DESEMBA 3, 2016.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua kiwanda cha Lodhia Plastic Industries
Limited kabala ya kukitembelea kiwanda hicho Desemba 3, 2016. Kulia ni
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo na kulia kwa Waziri Mkuu ni
Mwenyekiti wa Kampuni ya Nodhia Group, Haroon Lodhia.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa Kiwanda
cha Lodhia Plastic Industries Limited cha jijini Arusha, Haroon Lodhia
(kushoto ) kuhusu utengenezaji wa mabomba ya plastic wakati
alipotembelea kiwanda hicho,Desemba 3, 2016.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa kitazama matangi yanayotengenezwa katika kwanda
cha Lodhia Plastic Industries wakati alipokitembelea kiwanda hicho
Desemba 3, 2016 .
Waziri
Mkuu,Kasim Majaliwa akitazama gari linalotengenezewa bodi maalum kwa
ajili ya shughuli za utalii wakati alipotembelea kiwanda cha kutengeneza
mabodi ya magari cha HansPaul cha jijini Atusha Desemba 3, 2016.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa
kiwanda cha Fibreboards cha Arusha, Tosky Hans (wapili kulia) kuhusu
bidhaa zinazozalishwa na kiwanda hicho wakati alipokitembelea Desemba 3,
2016. Watatu kulia ni Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda
cha unga cha MONABAN cha Arusha wakati alipokitembelea Desemba 3, 2016
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama mfuko wenye unga wakati alipotembelea
kiwanda cha unga cha MONABAN jijini Arusha Desemba 3, 2016
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua shehena ya ungwa uliosindikwa wakati
alipotembelea kwanda cha unga cha MOBAN cha jijiniArusha Desemba 3,
2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Post a Comment