Dk 90+ 1: Yanga wanapata kona ya kwanza, lakini haina faida
Dk 87: Simba SC wanapata kona tena inazua kizaazaa langoni mwa Yanga kabla ya kuondoshwa kwenye hatari
Dk 82: Mashabiki wa Simba SC wanaanza kuachia siti zao Uwanja wa Taifa
Dk 80: Brian Majwega anakwedna kuchukua nafasi ya Ibrahim Hajib
Dk 72: Tambwe anaifungia Yanga bao la pili kwa guu la kulia akimalizia krosi ya Godfrey Mwashiuya kutoka kushoto
![]() |
| Amissi Tambwe anaifungia Yanga SC bao la pili Uwanja wa Taifa |
Dk 64: Godfrey Mwashiuya anakwenda kuchukua nafasi na Deus Kaseke
Dk 59: Danny Lyanga anachukua nafasi ya Hamisi Kiiza
Dk 52: Simon Msuva anachukua nafasi ya Haruna Niyonzima
Dk 46: Nova Lufunga anachukua nafasi ya Mwinyi Kazimoto
Dk 46: Kipindi cha pili kinaanza, Simba SC wanaukanyaga wakiwa pungufu baada ya Abdi Banda kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 25
![]() |
| Donald Ngoma ameifungia Yanga SC bao la kwanza Uwanja wa Taifa |
MPIRA NI MAPUMZIKO YANGA 1-0 SIMBA SC
Dk 45: Hassan Kessy anapiga mpira wa adhabu unapotea
Dk 44: Simba wanapata kona ya saba wanapoteza pia
Dk 44: Simba wanapata kona ya sita wanapoteza
Dk 39: Ngoma anaifungia Yanga bao la kwanza. Hassan Kessy alimrudishia pasi fupi kipa Vincent Angban, Ngoma akainasa akampga chenga kipa huyo na kufunga
Dk 35: Simba SC wanapata kona nyingine dakika ya 35, lakini inaokolewa
Dk 25: Abdi Banda anaonyeshwa kadi ya njano ya pili na kutolewa kwa kadi nyekundu kwa kumchezea rafu tena Ngoma
![]() |
| Refa Jonesia Rukyaa akimuonyesha kadi nyekundu Abdi Banda wa Simba SC |
Dk 20: Barthez ameinuka na mchezo unaendelea
Dk 18: Simba wanapiga kona nyingine, Barthez anacheza anaanguka na kupatiwa huduma ya kwanza
Dk 17: Simba wanapata kona ya tatu inazaa kona nyingine
Dk 14: Simba wanapata kona ya pili haina faida
Dk 8: Simba wanapata kona ya kwanza, lakini haina faida
Dk 1: Juuko anamchezea rafu Ngoma mpira unapigwa kwenda Simba
Saa 10:00: Mpira umeanza, wameanza Yanga
Saa 9:53: Timu ndiyo zinaingia uwanjani sasa
Saa 9:40: Timu zimemaliza kupasha misuli moto na zimerudi vyumbani tayari kuingia uwanjani tena kuanza mchezo
Vikosi;
Yanga SC: Barthez, Abdul, Bossou, Twite, Mngwali, Ngonyani, Kaseke, Kamusoko, Tambwe, Ngoma na Niyonzima.
Simba SC: Angban, Kessy, Tshabalala, Juuko, Banda, Majabvi, Mkude, Kazimoto, Kiiza, Hajib na Ndemla




Post a Comment