Pages

May 27, 2015

RAIS KIKKWETE ASEMA MISHAHARA YA WALIMU KUONGEZWA AGOSTI 1,2015

Walimu kutoka sehemu mbalimbali nchini wakiwa katika mkutano  wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) unaondelea jijini Arusha wakifuatilia kwa makini mada za mkutano huo .Picha na Ferdinand Shayo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mheshimiwa  Jakaya  Kikwete akiwasili katika ukumbi wa mkutano mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) unaoendelea  jijini Arusha .Jumla ya walimu 1000 walihudhuria mkutano huo kutoka sehemu mbalimbali nchini ambapo Rais Kikwete aliwahutubia na kuwaaga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete akiteta jambo na mmoja kati ya waasisi wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Thom Abieko jana wakati alipofungua mkutano mkuu wa chama hicho jijini Arusha.
Rais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete akisalimiana na walimu waliofika katika mkutano mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) unaoendelea  jijini Arusha .
Rais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete akisalimiana na walimu waliofika katika mkutano  wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT)

Walimu kutoka sehemu mbali mbali nchini waliohudhuria katika mkutano mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT)        



Na Ferdinand Shayo,Arusha.

Rais Jakaya Kikwete amesema kuwa walimu watarajie nyongeza ya mishahara itakayoanza mwezi Agosti mwaka huu ikiwa ni moja kati ya jitihada za serikali katika kuboresha maslahi ya walimu nchini.

Kikwete akihutubia Mkutano Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT ) uliofanyika jijini Arusha  amesema kuwa nyongeza hiyo itahusisha walimu wote wanaolipwa kima cha chini  cha mshahara na kima cha juu pasipo kutaja kiwango kilichoongezeka.

“Wakati mnachukua mishahara yenu benki mwezi Agosti mtaona tofauti ambayo ni nyongeza ya mshahara ,wenzenu wa chama cha Wafanyakazi waliniomba nisitangaze  niongeze kimya kimya ili wafanyabiashara wasipandishe bei ya bidhaa” alisema Rais Kikwete

Aidha Rais Kikwete amesema kuwa serikali inaendelea na jitihada za kuhakikisha kuwa inaboresha elimu nchini ikiwa ni pamoja na kuboresha maslahi ya walimu nchini,kuongeza vifaa vya kujifunzia na kufundishia,nyumba za walimu,vitabu  na maabara.

Amesema kuwa madai ya walimu wanayoidai serikali yatalipwa kwa awamu iwapo uhakiki utakamilika kwa sasa wanatarajia kulipa kiasi cha shilingi bilioni 7 kwa walimu 70100 watalipwa Agosti mwaka huu.

“Katika kufanya uhakiki wa madai ya walimu ikiwemo malimbikizo ya mishahara,posho za kufundishia,uhamisho tuligundua kuwa wako baadhi ya watu walifanya udanganyifu lakini sasa tunamalizia kufanya uhakiki ili fedha hizo zilipwe” Alisema Kikwete

Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Alhaji Yahaya Msulya amemtaka Rais Kikwete kushughulikia suala la posho ya kufundishia kwa walimu kwani walimu ni kundi linalofanya kazi kwa muda mrefu kuliko watumishi wengine wa serikali.

“Mwalimu anaingia shuleni saa 1:30 asubuhi anatoka saa 3:00 mda huo anatakiwa kusahihisha kazi za wanafunzi na kuandaa masomo ya kufundisha kesho hivyo anatumia muda mwingi sana katika kazi ni vyema serikali ikaliangalia suala hili” alisema Msulya

Katibu huyo ameupongeza uamuzi wa serikali kutoa bure elimu ya msingi na sekondari ambao utawasaidia watoto wengi hasa waliotoka kwenye familia zenye kipato cha chini.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...