Pages

January 15, 2015

Maazimio ya Kamati kuu CCM kwenye Kikao Z’bar haya hapa, Escrow, ishu ya Urais 2015 vimejadiliwa


Nape Nnauye
Kamati Kuu ya Halmashauri kuu ya CCM Taifa ilikuwa katika Kikao Kisiwandui, Zanzibar, kwenye ishu kubwa zilizojadiliwa zipo zinazohusu sakata la Escrow na pia ishu ya waliopewa adhabu kwa kukiuka maadili ya chama kwenye mchakato wa kugombea Urais 2015.
Katibu Mwenezi wa CCM, Nape Nnauye alitoa taarifa kuhusiana na maazimio ya CCM kuhusu ishu hizo; “Kamati kuu inaitaka Serikali na vyombo vinavyohusika kuendelea kutekeleza maazimio ya Bunge yaliyobaki, pili kamati kuu imewataka wale wote waliopewa dhamana wajenge utamaduni wa kuwajibika kwa dhamana zao na wasipowajibika, waliowapa dhamana wachukue hatua ya kuwawajibisha.
Kwamba kutokana na sakata hili na jinsi lilivyokwenda Kamati Kuu inataka wanopewa dhamana wajenge utamaduni wa kuwajibika inapotakiwa kuwajibika na wasipowajibika wao wale waliowapa dhamana wachukue hatua za kuwawajibisha
Kamati Kuu imeiagiza Kamati ndogo ya Maadili kuchukua hatua za kimaadili  kwa wale wote waliohusika na ukiukwaji wa maadili katika sakata la Escrow, ambao wako kwenye vikao vya maamuzi vya chama katika sakata hili wako viongozi wetu wa chama, ambao wapo kwenye vikao vya maamuzi kwa maana ya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu na kwa namna moja ama nyingine wamehusishwa kwenye sakata hili na vitendo vyao vimehusishwa na ukiukwaji wa maadili“– Nape Nnauye.
Makada 6 wa CCM waliopewa adhabu kwa kuhusishwa na ukiukwaji wa maadili kwenye mchakato wa kutaka kuteuliwa na CCM kugombea Urais, watamaliza muda wa adhabu zao Mwezi wa pili mwaka huu 2015… itafanyika tathimini kuona kama walizingatia masharti ya adhabu zao na kama kuna ambao watakutwa hawakuzingatia masharti ya adhabu zao au wamefanya matendo ya ukiukwaji tena wa maadili wataongezewa adhabu“– Nape Nnauye.
Nape aliwatangaza waliopewa onyo hilo kuwa ni Edward Lowassa, Frederick Sumaye, January Makamba, Steven Wassira, Benard Membe na William Ngeleja.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...