Pages

September 11, 2014

Kilichosemwa na Mahakama leo kuhusu kesi ya Oscar Pistorius Afrika Kusini


Screen Shot 2014-09-11 at 2.13.03 PMOscar Pistorius ni mwanariadha wa Afrika Kusini ambae amekua kwenye headlines kutokana na ishu yake ya kutuhumiwa kumuua mpenzi wake kwa risasi Valentine’s day mwaka jana.
Taarifa mpya za Mahakama leo zinasema Jaji ametoa maamuzi kwenye shitaka la kwamba alifanya mauaji ya kukusudia, amesema upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha.
Kwenye kesi hii Pistorius alikiri kumuua mpenzi wake lakini ni kwa bahati mbaya na sio makusudi ambapo Mwandishi wa BBC ameripoti kwamba huenda Jaji akachukua mpaka Ijumaa kukamilisha maamuzi yake.
Ikitokea Pistorius akapatikana na hatia ya kumuua mpenzi wake basi anaweza kufungwa jela miaka 25. 

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...