Pages

October 20, 2013

RAIS JAKAYA KIKWETE NA MAMA SALMA WATEMBELEA WILAYA ZA WANGING'OMBE NA MAKETE,MKOANI NJOMBE


Rais Jakaya Kikwete akikata utepe ikiwa ni ishara ya kuzindua rasmi Chuo cha VETA cha Wilaya ya Makete tarehe 19.10.2013 kilichojengwa katika Mji wa Iwawa, Makao Makuu ya wilaya hiyo. KatIka hafla hiyo uongozi wa Chuo hicho umeamua kukipa jina la Jakaya Kikwete kwa jitihada zake alizowezesha wilaya ya Makete kuwa ya kwanza nchini kuwa na chuo cha VETA cha wilaya. Kulia kwa Rais Kikwete ni Waziri wa Elimu NA Ufundi Dr. Shukuru Kawambwa na kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Makete Ndugu Josephine Matiro.
Rais Jakaya Kikwete akifuatana na Mkewe Mama Salma wakitembelea Chuo cha VETA cha Makete na kuangalia shughuli mbalimbali zinazofanywa na wanachuo wa chuo hicho mara tu baada ya kukizindua rasmi tarehe 19.10.2013. 
Rais Jakaya Kikwete na Mama Salma wakipata maelezo ya namna gani ya kupata udongo unaofaa kwa ajili ya kufyatua matofali kutoka kwa Geofrrey Sanga na Abel Mbilinyi, wanachuo wa mwaka wa kwanza wa chuo hicho.
Rais Jakaya Kikwete akiteta jambo na baadhi ya Mawaziri aliofuatana nao katika ziara yake ya kuutembelea Mkoa wa Njombe wakati aliposimama katika kijiji cha Kipengere huko Wanging’ombe kukagua mambo ya maendeleo na pia kusalimiana nawananchi tarehe 19.10.2013.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na Paroko wa Kanisa Katoliki wa Parokia ya Kipengere iliyoko katika Wilaya ya Wanging’ombe , Mkoani Njombe wakati Mama Salma alipowasili kijijini hapo tarehe 19.10.2013 akifuatana na Rais Jakaya Kikwete anayetembelea Mkoa wa Njombe.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...