![]() |
| Wafanyakazi wa Jumuiya ya Afrika(EAC)wakipita kwa matembezi kwenye mitaa ya jiji la Arusha katika maadhimisho ya Siku ya wanawake kimataifa yaliyofanyika jana.Picha na Filbert Rweyemamu |
![]() |
| Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ),Monduli mkoa wa Arusha wakiongoza matembezi ya maadhimisho ya siku ya Wanawake kimataifa yaliyofanyika makao makuu ya jumuiya ya Afrika Mashariki(EAC) |
![]() |
Wafanyakazi wa Jumuiya ya Afrika(EAC)wakipita kwa matembezi kwenye mitaa
ya jiji la Arusha katika maadhimisho ya Siku ya wanawake.
|
![]() |
| Wafanyakazi wa Jumuiya ya Afrika(EAC) na wananchi wakipita kwa matembezi kwenye mitaa ya jiji la Arusha. |
![]() |
| Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika(EAC),Utawala na Fedha,Jesca Eriyo akizungumza katika eneo la Soko Kuu jijini Arusha. |
![]() |
| Afisa Rasilimali Watu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki(EAC),Ruth Simba akishiriki kufanya usafi kwenye Soko Kuu la Jiji la Arusha |
![]() | ||||||||
| Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika(EAC),Utawala na Fedha,Jesca Eriyo aliyeinua mkono juu zaidi akizungumza katika eneo la Soko Kuu jijini Arusha. |
Filbert Rweyemamu
Arusha.Naibu
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki(EAC) anayeshughulikia
Utawala na Fedha,Jesca Eriyo amekosoa mfumo dume unaozuia idadi kubwa ya
wanawake kuwa katika nafasi za maamuzi.
Akizungumza
katika maadhimisho ya siku ya Wanawake duniani yaliyofanyika
katika Soko Kuu la jiji la Arusha alisema haoni sababu za wanawake
kuendelea kufanyakazi za chini wakati wanaweza kufanya kazi zote za
kitaalamu.
"Mfumo
dume umetawala sana na mgumu kuuvunja hasa kwetu waafrika,katika
Jumuiya ya Afrika Mashariki niko mwanamke pekee kati ya wanaume sita
kwenye ngazi ya juu ya menejimenti,vilevile hata ngazi ya Wakurugenzi
yupo mwanamke mmoja huku wanaume wapo saba,"alisema Eriyo
Maadhimisho
yao yaliandaliwa na wanawake wanaofanya kazi jumuiya ya Afrika
Mashariki kwa kushirikiana na asasi za wanawake na vijana zinazohusika
na harakati za kuyajengea uwezo makundi hayo.
Naibu
Katibu Mkuu huyo aliwaongoza wanawake kufanya usafi na kukabidhi vifaa
mbalimbali vya usafi kwa jiji la Arusha ili kusaidia juhudi za kuuweka
mji huo katika hali ya usafi wakati wote.
"Tumetoa
vifaa hivi hasa vya usalama ili kuwawezesha wanawake ambao wengi wao
ndio wanaofanya kazi za usafi wawe salama kiafya ili kuendelea kusaidia
familia zao,"alisema Eriyo
Naye
Mratibu wa taasisi ya Widows Empowerment and HIV/AIDS
Foundation(WEHAF),Halima Mohamed alisema maadhimisho ya siku ya wanawake
duniani ina maana kubwa kwani inawaleta pamoja wanawake kujadili
changamoto zinazowakabili na kuzipatia ufumbuzi.
"Wanawake
wengi wameachiwa majukumu ya kutunza familia na ukizingatia mfumo dume
uliwanyima elimu kwahiyo wanafanya kazi ngumu na zenye malipo duni
sana,"alisema
Kwa
upande Afisa Mipango Miji wa Jiji la Arusha,Mariam Kimolo alisema
wanawake wana mchango mkubwa katika ustawi wa familia na taifa kwa
ujumla na serikali inatambua mchango kwa kuwapa nafasi za uongozi.








إرسال تعليق