TAHA YAPANIA KUKUZA BIASHARA YA MAUA NA MATUNDA NCHINI

Mwenyekiti wa Bodi ya Tanzania Horticulture Association(Taha) Eric Ng’imaryo(katikati) akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha kujadili mikakati ya kuinua sekta ya wazalishaji wa mazao ya bustani nchini,kushoto ni Mwenyekiti mstaafu,Colman Ngalo na Mkurugenzi wa Taha,Jackline Mkindi.

Mwenyekiti Mstaafu wa Bodi ya Tanzania Horticulture Association(Taha)Wakili Colman Ngalo akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha kujadili mikakati ya kuinua sekta ya wazalishaji wa mazao ya bustani nchini,katikati ni Mwenyekiti mpya,Eric Ng’imaryo na Mkurugenzi wa Taha,Jackline Mkindi

Mwenyekiti wa Bodi ya Tanzania Horticulture Association(Taha) Eric Ng’imaryo akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha kujadili mikakati ya kuinua sekta ya wazalishaji wa mazao ya bustani nchini,kushoto ni Mkurugenzi wa Taha,Jackline Mkindi.     

Mwandishi Wetu,Arusha.
Mwenyekiti  wa Bodi ya Tanzania Horticulture Association(Taha),Eric Ng’imaryo amesema ili kilimo cha Maua,mbogamboga na viungo kiweze kuleta tija kwa wananchi kama ilivyo katika nchi nyingine serikali inapaswa kuweka sheria madhubuti za  umilikaji wa ardhi unaoaminika.

Akizungumza  baada ya kikao cha bodi kilichokua kikijadili kwa kina namna ya kukuza kiwango na ubora wa mazao hayo alisema iwapo sheria itakua wazi basi kilimo cha bustani za mazao hayo kitawanufaisha wananchi wengi.

Alisema Taha itaendelea kutoa mafunzo ya mashamba darasa kwa wakulima wenye mashamba madogo ambayo yakitumiwa ipasavyo yanaweza kubadilisha maisha ya wakulima badala ya kuona kilimo cha bustani za maua ni kwaajili tu ya wawekezaji kutoka nje ya nchi.

Kwa upande Mwenyekiti  wa Bodi aliyemaliza muda wake,Wakili Colman Ngalo alisema serikali inatakiwa kuboresha mazingira ya uwekezaji kwa kupunguza urasimu ili kufungua milango kwa uwekezaji mkubwa katika sekta ya maua na mbogamboga nchini.

Alisema Tanzania ni moja ya nchi zilizojaliwa kuwa na maeneo makubwa ya ardhi na yenye rutuba kwamba kilimo cha bustani hakina budi kufanyika kwa manufaa makubwa.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taha,Jackline Mkindi alisema taasisi yake imekua ikitoa mafunzo kwenye vyuo mbalimbali vikiwemo vyuo vikuu ya Sokoine cha Morogoro na Saint Augustine cha mkoani Mwanza kwa vijana  namna ya kujiingiza na kuendesha kilimo cha bustani pindi wanapomaliza masomo yao.

Alisema vijana ni sehemu muhimu katika kuendeleza kilimo hicho kwani idadi yao ni kubwa na wana nguvu ya kusimamia hadi kufikia malengo yao .

Mkindi alisema sekta ya kilimo cha bustani imepiga hatua ambayo imechangiwa kwa kiwango kikubwa na vyombo vya habari na mwaka huu Taha itaanzisha Tuzo kwa waandishi bora wanaoandika na kuhamasisha sekta hiyo nchini.

Post a Comment

Previous Post Next Post