Pages

June 22, 2013

ARUSHA TECHNICAL COLLEGE(ATC)WASHEREKEA SIKU YA FAMILIA


Mkuu wa Chuo cha  Arusha Technical College(ATC)Dk Richard Masika akizungumzia  na waandishi wa habari  juu ya umuhimu siku ya familia ya chuo hicho iliyofana sana  na kuwa ni njia  kuongeza ushirikiano baina ya wafanyakazi na familia zao

Moja ya huduma ya kibenki iliyokuwepo uwanjani kutoa huduma kwa wanafamilia wa ATC

Watoto wa wafanyakazi chuo hicho wakifurahia siku ya leo

Watoto wa wafanyakazi chuo hicho wakifurahia siku ya leo


Makamu Mkuu wa Chuo,Dk Mgaya(wa pili kulia)akitoa maelezo kabla ya mchezo wa mpira wa miguu kati ya timu ya Utawala na Civil Engenering 

Wanafamilia wakiingia kwenye eneo la tukio kufurahia pamoja siku ya wanafamilia

Michezo mbalimbali ilikuwepo kama Netball kwa kuwajumuisha watu wa rika mbalimbali

Mchezo wa Vollebal ulikua miongoni mwa michezo iliyovutia wanafamilia wa ATC

Katika kujali afya za wanafamilia Chuo kilitoa nafasi ya kupima afya ikiwa pamoja na kupima uzito,mapigo ya moyo,Sukari,na Ukimwi kwa hiari

Kama kawaida maeneo kama haya maakuli ni sehemu muhimu sana hayawezi kuwa mbali hapa wahudumu wakiandaa sahani

Na Mwandishi Wetu,Arusha
Wanafamilia wa Chuo cha Ufundi Arusha leo wamekua na siku ya kuburudika pamoja kwa kushiriki michezo mbalimbali iliyofanyika katika viwanja vya chuo hicho.

Mkuu wa Chuo hicho,Dr Richard Masika amesema siku hii inawapa nafasi wanafamilia kubadilishana mawazo,kujumuika kwenye michezo ya aina mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu,mchezo wa Netball,Vollebal,kukimbiza kuku,kuvuta kamba nk ili kuwapa nafasi ya kuimarisha afya zao.

Amesema fursa hii ni pekee kwa wanafamilia hao kuboresha mahusiano yao na wale walikosena kusameana na kuanza upya lengo likiwa kukuza umoja miongoni mwao.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...