Arusha.Jumuiya
ya Afrika Mashariki(EAC) kwa kushirikiana na shirika la maendeleo la
kimataifa la Ujerumani(GIZ) kupitia mradi wa kudhibiti na kupambana na
magojwa ya mlipuko utawakutanisha wadau na wataalamu wa afya kujifunza
mikakati ya kukabiliana na magonjwa hayo baada ya uzoefu walioupata
kwenye nchi za Afrika Magharibi.
Watalaamu
mbalimbali 500 kutoka nchi za Afrika Mashariki mwaka 2014 na 2016
walienda katika nchi za Afrika Magharibi kusaidiana na watalaamu wa afya
kupambana na ugonjwa hatari wa Ebora ambao ulisababisha vifo vya watu
na kuacha makovu.
Taarifa
iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Mkuu wa Mawasiliano wa EAC,Richard
Owora ilisema tangu wataalamu hao tangu warejee kwenye nchi zao
utaalamu,maarifa na uzoefu walioyapata haujawekewa mfumo maalumu wa
kuuweka kwenye maandishi kwaajili ya kuutumia pindi milipuko hiyo
itakapotokea kwenye nchi za EAC.
"Kwa
kushirikiana na wadau wa maendeleo ambao ni GIZ na benki ya maendeleo
ya Ujerumani(KfW) Novemba 6 hadi 8 mwaka huu tutawakutanisha watalamu
hao nchini Kenya kuona namna tunavyoweza kutumia maarifa ya wenzetu
waliojitoa mhanga kwenda kuokoa maisha ya ndugu zetu kuona namna
tunavyoweza kuyatumia wakati ujao," ilisema taarifa hiyo
Mkutano
huo utasaidia kuhakikisha nchi za Afrika Mashariki zinakua na uwezo wa
kujiandaa kukabiliana na magonjwa ya milipuko na yanayoambukizwa ili
kulifanya eneo zima la EAC kuwa salama.
Mwaka
2014 hadi 2016 nchi za Liberia,Guinea na Siera Leone zilishambuliwa na
ugonjwa wa Ebola ambao ulisababisha vifo vya watu na kuathiri mfumo wa
kiuchumi wa nchi hizo.
Mganga
Mkuu wa Jiji la Arusha,Dk Simon Chacha alisema mkutano huo utazisaidia
nchi za Afrika Mashariki kujenga uwezo wa kukabiliana na magonjwa ya
mlipuko na yanayoambukiza ili kuhakikisha nchi zote zinakua tayari
kukabiliana magonjwa hayo.

Post a Comment