Pages

January 18, 2017

MWIJAGE AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KIWANDA CHA SABUNI MKOANI PWANI

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akizindua Jiwe la Msingi la Kiwanda Keds.kwakushirikina na Mkurugenzi wa Kiwanda hiko, Jack Feng.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage ameweka jiwe la msingi kuashiria kuanza kwa ujenzi wa Kiwanda cha Sabuni (Keds) kilichopo Kibaha Mkoani Pwani.

Kiwanda hicho ni cha pili kujengwa katika Bara la Afrika baada ya cha kwanza kujengwa nchini Ghana.

Akizungumza wakati wa uwekaji wa jiwe hilo,Waziri Mwijage amesema kuwa amefurahi kuona mapambano yakuendeleza Tanzania ya Viwanda,amesema kupitia ujenzi wa Viwanda hivyo ukuaji wa Uchumi utakuwa sambamba na ukuaji wa Maendeleo ya Watu.

Pia amesema kuwa Kiwanda hiko cha Keds kimeitoa Tanzania kimasomaso katika kutimiza asilimia 40 ya upatikanaji wa ajira pamoja na kuziomba Mamlaka za Mikoa kote nchini kuiga Mfano wa Pwani katika Uwekezaji wa Viwanda na kujifunza ukarimu kwa wawekezaji.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC),Clifford Tandari amesema kuwa ni fursa muhimu kwa kuwa Kampuni hiyo tayari ina Kiwanda Ghana hivyo kujengwa Tanzania kitakuwa cha pili.

Amesema kuwa baada ya Kiwanda hicho kuisha kitaokoa gharama za uingizaji wa sabuni kutoka nje.

Naye Mkurugenzi wa Kiwanda hiko, Jack Feng,amesema tangu kuanza kwa mradi huo wametumia muda mfupi kuweka sawa ardhi ya eneo hilo pia amesema kuwa watajenga kwa uzoefu na ujuzi ili kutimiza azma ya uwekezaji bora Tanzania.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akizungumza wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi kuashiria ujenzi wa Kiwanda cha Keds kilichopo Kibaha Mkoani Pwani.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Nchini, Clifford Tandari akizungumza wakati wa uwekwaji wa jiwe la msingi katika Kiwanda cha Sabuni cha Keds.
Mkurugenzi wa Kiwanda hiko, Jack Feng akizungumza wakati wa uwekwaji wa jiwe la msingi katika Kiwanda cha Sabuni cha Keds.
Baadhi ya viongozi mbalimbali na wanachi wakimsikiliza Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji,Mhe Charles Mwijage wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi kuashiria ujenzi wa Kiwanda cha Sabuni(Keds) kilichopo Kibaha Mkoani Pwani.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akiagana na Mkurugenzi wa Kiwanda hiko,Jack Feng baada ya kuwasili katika Mkoani Pwani.katikani Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Nchini,Clifford Tandari
Muonekano wa Mchoro kiwanda namna kitakavyo kuonekana baada ya kukamilika ujenzi wake.







No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...