Pages

December 3, 2016

TIB CORPORATE BANK YATOA SH 20 MILIONI KUWASAIDIA VIJANA JIJINI ARUSHA

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mheshimiwa Kassim Majaliwa(kushoto)akipokea mfano wa hundi wenye thamani ya Sh 20 milioni kutoka kwa Meneja wa TIB Corperate Bank Limited tawi la Arusha,Juliana Mwansuva(kulia)ukiwa ni mchango wa benki hiyo kwaajili ya kununua Pikipiki ambazo Waziri Mkuu amezikabidhi leo kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha wanaoshudia kutoka kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo,Mkurugenzi Mkuu wa TIB Corperate Bank,Frank Nyabundege na Waziri wa Maliasili na Utalii,Profesa Jumanne Maghembe.

Meneja wa TIB Corperate Bank Limited tawi la Arusha,Juliana Mwansuva(kulia)akipongezwa na Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo baada ya kumkabidhi Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mheshimiwa Kassim Majaliwa(kushoto) mfano wa hundi wenye thamani ya Sh 20 milioni kwaajili ya kununua Pikipiki .

Baadhi ya walionufaika na Pikipiki zilizotolewa na Waziri Mkuu ambazo zilichangiwa na wadau mbalimbali mkoani Arusha,mradi huo utawawezeha vijana kurejesha fedha zenye thamani ya Pikipiki kisha kuwa wamiliki halali.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mheshimiwa Kassim Majaliwa na Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo wakizungumza na mmoja wa watu wenye ulemavu walionufaika na msaada wa Pikipiki leo.

Pikipiki mpya zaidi ya 200 zenye thamani ya Sh 400 milioni zilizotolewa kwa vijana jijini Arusha leo katika ziara ya Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...