Pages

May 28, 2016

WANANCHI WAFURIKA BANDA LA BENKI YA NMB KATIKA MAONESHO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI UWANJA WA CHUO KIKUU CHA USHIRIKA MOSHI.

Mgeni Rasmi katika Maonesho ya Wakulima na Wafugaji,Mkuu wa Idara ya Utumishi na Utawala manispaa ya Moshi,Wencelaus Lindi akitia saini katika kitabu cha wageni mara baada ya kutembelea banda la Benki ya NMB katika maeonesho hayo yanayofanyika katika uwanja wa Chuo Kikuu cha Ushirika mjini Moshi.
Meneja Mwandamizi wa Mahusiano ya biashara na Kilimo wa Benki ya NMB,Oscar Rwechungura (aliyenyoosha kidole) akitoa maelezo kwa mgeni rasmi ,Wencelaus Lindi (aliyekunja mikono) katika maonesho ya Wakulima na Wafugaji yaliyoandaliwa na Mtandao wa kusaidia wakulima wa AgriProFocus.
Meneja wa Benki ya NMB tawi la Nelson Mandela mjini Moshi,Emanuel Kashusho akikabidhi zawadi ya T-shirt ,Kalamu na Key holder kwa mgeni rasmi ,Wencelaus Lindi mara baada ya kutembelea banda la Benki hiyo na kupata maelezo namna inavyoshirikiana na wakulima katika kukuza mitaji yao.
Mgeni rasmi ,Wencelaus Lindi akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya NMB pamoja na wananchi wengine waliofika kutembelea banda la NMB.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...