Pages

November 11, 2015

Trump ashutumiwa kwa kupanga kufurusha wahamiaji





Donald Trump, mmoja wa wanaowania kupeperusha benderea ya chama cha Republican uchaguzini Marekani, ameshutumiwa vikali kutokana na mpango wake wa kuwafurusha wahamiaji 11 milioni kutoka Marekani.

Kwenye mdahalo wa moja kwa moja kupitia runinga, wawaniaji wawili wanaoshindana naye, John Kasich na Jeb Bush, walikosoa vikali mpango huo wakisema hauwezi kutekelezeka.

Aidha, wamesema ni wa ubaguzi na wenye nia ya kuzua mgawanyiko kwenye jamii.
Bw Trump, ambaye ni bilionea kutoka New York, alizomewa alipojaribu kujitetea.
Wagombea wanane wanaoongoza kwenye chama hicho walikabiliana Milwaukee kwa mara ya nne.

Bw Trump alikariri mpango wake wa kujenga ua katika mpaka wa Marekani na Mezico kuzuia wahamiaji kuingia Marekani na pia kuhakikisha wahamiaji walioingia Marekani kinyume cha sheria wanafurushwa na kurejeshwa Mexico.

Lakini alikosolewa vikali na Bw Kasich, ambaye ni gavana wa Ohio.
"Tuseme ukweli, sote tunajua huwezi ukawashukua na kuwarejesha kwao vivi hivi tu. Hilo ni wazo la kijinga. Si wazo komavu.”

Bw Bush, aliyekuwa gavana wa Florida, pia alishutumu mpango huo akisema utatenganisha familia.

Lakini Trump alitetea msimamo wake na kusema wahamiaji hao wanadhuru uchumi wa Marekani.

Daktari wa upasuaji Ben Carson amekuwa akimfuata kwa karibu Donald Trump kwenye kinyang’anyiro hicho kwa mujibu wa kura za maoni.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...