Ishu ya viongozi na wanachama wa CHADEMA kuzuiwa kuaga mwili wa Marehemu Alphonce Mawazo, aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama hicho Geita imekuwa ikiripotiwa na kuandikwa kwenye vyombo vya habari huku ikisubiriwa kutolewa majibu na Mahakama Kuu Mwanza kuhusu hatma ya zuio hilo.
Leo maamuzi ya Mahakama Kuu Mwanza
yametoka na majibu kwamba wanaCHADEMA na viongozi wao wamepata kibali
cha Mahakama hiyo kuendelea na shughuli za kuaga pamoja na mazishi ya
kiongozi huyo.
Nje ya Mahakama Kuu Mwanza, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Aikael Mbowe alipata dakika chache kuongea na wanachama wa CHADEMA ambao walikuwa wakisubiri kusikia maamuzi ya Mahakama >>>> “Ni
lazima tukae vikao kupanga ratiba ya kumuaga Kamanda Mawazo, Jaji
ametoa maelekezo kwamba viongozi wa CHADEMA, familia ya marehemu na
Jeshi la Polisi wakae pamoja kupanga ratiba kamili.”
“Tutaheshimu
maelekezo ya Jaji lakini hatutakubali kuonewa, muwe na imani kwamba
haki itatendeka… tunakwenda kwenye vikao lakini tunahitaji kumaliza
jambo hili kuanzia kesho, tutamuaga Mawazo kwa heshima anayostahili
katika eneo ambalo tutawatangazia.” >>> Freeman Mbowe.
No comments:
Post a Comment