Pages

October 7, 2015

DK. Shein Aendelea na Mikutano yake ya Kampeni Zanzibar Akiwahutubia Wananchi wa Bumbwini

Mama Fatma Karume akishuka jukwaani baada ya kuwahutubia Wananchi na Wana CCM katika viwanja vya mpira bumbwini makoba wakati wa mkutano wa Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, mkutano uliofanyika katika Jimbo la Bumbwini Unguja.
Mgombea wa Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akimpongeza Mama Fatma Karume baada ya kuwahutubia Wananchi na kumuombea Kura kwa Wananchi wakati wa Mkutano huo wa Kampeni katika Wilaya ya Kaskazini B uliofanyika viwanja vya mpira bumbwini makoba.
Umati wa Wanachama wa CCM wakiwa katika viwanja vya mpira bumbwini makoba wakihudhuria mkutano wa mgombea wa CCM Dk Ali Mohamed Shein. 
Mbunge wa Jimbo la Mpendae Mhe Salim Turky (Mr White) akiwa katika mkutano wa mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, uliofanyika katika viwanja vya bumbwini makoba wakimsikiliza Mgombea.
Mwakilishi wa Jimbo la Tumbatu Mhe Haji Omar Kheri akiwahutubia Wananchi katika mkutano wa kampeni ya Mgombea wa CCM Dk Shein, katika viwanja vya bumbwini makomba na kumuombea Kura Dk Shein, ili kuendeleza amani na utilivu na Masendeleo ya Wazanzibar.
Kada wa CCM Balozi Amina Salim Ali akiwahutubia Wananchi na Wanachama wa CCM katika mkutano wa kampeni ya Mgombea wa CCM Dk Shein 
Baadhi ya Wagombea wa CCM wakifuatilia mkutano wa Mgombea wa Urais wa Zanzibar kupitia CCM Dk. Ali Mohamed Shein, uliofanyika Wilaya ya Kaskazini B Unguja katika viwanja vya mpira bumbwini makoba.
Kijana wa CCM akitowa maelezo kwa Ishara kwa ajili ya Watu wenye ulemavu wa kutosikiwa wakati Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akihutubia mkutano huo na kutowa Sera za CCM kwa kipindi cha miaka mitano ijayo baada ya kupata ridhaa za Wananchi kumpigia kura kuongoza kwa mara ya Pili katika nafasi yake hiyo ya Urais wa Zanzibar.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiwahutubia Wananchi wa Mkoa wa Kaskazini na kueleza mafanikio yaliotekelezwa na Dk Shein, katika kipindi chake cha miaka mitano inayomalizika na kuelezea Ilani ya CCM kwa miaka mitano ijayo.
WanaChama wa CCM wakimshangilia wakatin wa mkutano huo wa kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar.
Msanii Msechu akitowa buridani kwa Wanachama wa Chama cha Mapinduzi wakati wa mkutano wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, katika viwanja vya bumbwini makoba Unguja.
                                                                    Mchechu ndani ya Zenj 
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akiwahutubia Wananchi katika mkutano wake wa Kampeni uliofanyika katika viwanja vya mpira bumbwini makoba Unguja na kuwataka wananchi kumpigia kura ya ndio kuiongoza Zanzibar kwa mara ya pili kuendeleza Mafanikio kwa Wananchi wa Zanzibar katika Sekta mbalimbali za Uchumi Zanzibar. 

Wanachama wa CCM wakimshangilia Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, wakati akiwahutubia na kuelezea Ilani ya CCM ya Uchaguzi kwa miaka mitano ijayo.
Mwanachama wa CCM akifuatilia hutuba ya Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohame Shein, wakati wa mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya bumbwini makoba Wilaya ya Kaskazini B Unguja.
Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM Dk. Ali Mohamed Shein, akiwatambulisha wagombea wa CCM nafasi za Ubunge katika Wilaya ya Kaskazini B Unguja wakati wa mkutano wake wa kampeni uliofanyika viwanja vya bumbwini makoba Unguja.
Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM Dk. Ali Mohamed Shein, akiwatambulisha wagombea wa CCM nafasi za Uwakilishi katika Wilaya ya Kaskazini B Unguja wakati wa mkutano wake wa kampeni uliofanyika viwanja vya bumbwini makoba Unguja.
Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM Dk. Ali Mohamed Shein, akiwatambulisha wagombea wa CCM nafasi za Udiwani katika Wilaya ya Kaskazini B Unguja wakati wa mkutano wake wa kampeni uliofanyika viwanja vya bumbwini makoba Unguja.
Wanachama wa CCM wakimshangilia Mgombea wa Urais wa Zanzibar Dk Shein, wakati akiwahutubia katika viwanja vya bumbwini makoba Unguja akiwa katika mikutano yake ya Kampeni Zanzibar. 
Viongozi wa CCM na Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, wakiitikia dua iliokuwa ikisomwa na Mzee wa Kijiji cha Bumbwini Makoba baada ya kumalizikika kwa mkutano wa Kampeni ya Urais wa Zanzibar katika viwanja vya Mpira Bumbwini Makoba Wilaya ya Kaskazini B Unguja.

Imetayarishwa na Othmanmapara.Blogspot, Zanzinews.com

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...