Pages

April 29, 2015

Mayweather na msafara wake kwenda kukagua Uwanja watakapopigana

Siku mbili tu zimesalia kabla ya pambano la kimataifa la ngumi kati ya mastaa wawiliManny Pacquiao na Floyd Mayweather ambao watapanda ulingoni na kutegua kitendawili cha nani mkali zaidi.
Hili pambano ni kama dunia nzima inalisubiri kwa hamu yani.. vyombo vya habari vimelipa promo kubwa kiasi cha kwamba hata ambao hawafuatilii ndondi imebidi wafuatilie hawa jamaa ni akina nani hasa !!
Jana nilikusogezea pichaz zikionesha Manny Pacquiao akiingia zake Las Vegas na msafara kabisa wa pikipiki, basi kubwa na gari nyingine zikimsindikiza.
Leo ni zamu ya Floyd Mayweather ambaye ametumia muda wake kwenda kukagua ukumbi wa MGM Grand ambao utatumika kwa pambano lao.
Ukumbi ulifurika mashabiki.. camera za mapaparazzi nazo hata hazikuwa mbali.
Pambano hilo linatajwa kuwa pambano la kifahari zaidi duniani na ambalo viingilio vyake ni vikubwa ukilinganisha na mapambano mengine yaliyowahi kufanyika duniani.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...