Pages

April 26, 2015

KIONGOZI WA CHADEMA NA UKAWA FREEMAN MBOWE ANGURUMA MKOANI SIMIYU

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, akizungumza na halaiki ya vijana wa chama hicho muda mfupi baada ya kuifunga kambi ya mafunzo ya vijana hao iliyofanyika Kijiji cha Lagangabilili Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu juzi.
Mamia ya wananchi wa Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu, wakimshangilia Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe (hayupo pichani), katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Sekondari Lagangabilili wilayani humo juzi.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, akihutubia mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Lagangabilili Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu juzi.
Wazee wa kabila la wasukuma wakimuombea kwa Mwenyezi Mungu, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, ili yeye na chama chake aweze kutawala nchi. Mbowe alisimikwa na kupewa zana za kitemi za kabila hilo na kuitwa jina la Mayego kabla ya kuanza kuhutubia mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Kijiji cha Lagangabilili wilayani Itilima mkoani Simiyu juzi.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...