Hii ishu imechukua headlines kwenye mitandao ya kijamii ambapo wengine hawakuwa na taarifa kamili kuhusu tukio lenyewe, nikaifatilia kwa ukaribu na kupata taarifa kamili kupitia kwenye blog ya Issamichuzi ambayo imekua ikifanya vizuri kwenye utoaji wa habari.
Ishu inahusu tukio la ujambazi ambalo limetokea leo Kinondoni Dar es salaam ambapo majambazi wanne wamemvamia na kumpora mtu mmoja ambae ni raia wa kigeni (mzungu) na kisha wakakimbia.
Sasa kwa ufupi ilivyokuwa kuna mtu aliwafatilia mpaka eneo la mataa ya Red Cross na gari yake alafu akawablock ambapo Askari tayari waliopewa taarifa wakafanikiwa kuwakamata wakiwa na bunduki mbili.
No comments:
Post a Comment