Rais
wa
Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu(AfCHPR)Jaji Augustino
Ramadhani(wa pili kulia)akiwa katika picha ya pamoja na Naibu
Mwakilishi Mkazi wa taasisi ya kimataifa
“La Francophonie” katika Umoja wa Afrika(AU)yenye makao yake Addis
Ababa,Ethiopia,Cecile Leque Folchini(kulia)kushoto ni Msajili wa
mahakama hiyo,Dk Eno Robert na Mkurugenzi wa Alliance Francaise
d'Arusha,Gaelle Lapostolle.
Mwandishi Wetu
Rais
wa
Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu(AfCHPR)Jaji Augustino
Ramadhani leo amefanya mazungumzo na Naibu
Mwakilishi Mkazi wa taasisi ya kimataifa
ya “La Francophonie” katika Umoja wa Afrika(AU)yenye makao yake Addis
Ababa,Ethiopia,Cecile Folchini kwenye ofisi za Mahakama ya Afrika
jijini Arusha ambayo yamejikita kushirikiana baina ya taasisi hizo mbili.
Cecile alisema taasisi yake iko mbioni kuona ni namna gani wataisaidia Mahakama hiyo ya Afrika ya Haki za Binadamu ili kuiwezesha kufanya kazi zake ipasavyo.
Katika ujumbe wake aliambatana na Mkurugenzi wa Alliance Francaise d'Arusha,Gaelle Lapostolle ambayo hutoa mafunzo ya kifaransa ambayo iliahidi kutoa mafunzo kwa Majaji wa Mahakama hiyo kujifunza kifaransa katika muda wao wa ziada.
Mahakama hiyo ina Majaji kutoka nchi mbalimbali zikiwemo zisizotumia lugha ya kifaransa kama lugha rasmi zikiwemo Afrika Kusini,Tanzania,Uganda,Malawi na Kenya.
Lugha rasmi za Mahakama hiyo ni Kiingereza,Kifaransa,Kireno na Kiarabu. |
No comments:
Post a Comment