Pages

February 6, 2015

GHANA 3-0 EQUATORIAL GUINEA AFCON 2015 GHANA KUCHEZA NA IVORY COAST FINAL JUMAPILI.

 wachezaji wa Ghana  wakishangilia ushindi na kutinga fainali baada ya kuwakunja wenyewe Equatorial Guinea 3-0  kwahiyo sasa  Ghana kukutana na Ivory Coast tarehe 8 kwenye fainali. 
Baada ya kipenga cha mwisho wenyeji wa mashindano hayo ya AFCON walikuwa wamekubali kipigo cha magoli matatu ndipo washabiki walivyoanzisha timbwili hili uwanjani hapo.
Hali ilionekana siyo shwari toka kipindi cha kwanza pale Ghana walivyopewa penati ya mapema hii hapa ilikuwa baada ya dk 45 za kwanza washabiki wenye mizimu ya kinyamulenge walianza kuwarushia makopo na chupa wacheza wa Ghana walivyokuwa wakielea kwenye vyumba vya mapumzikia.
Uwanjani hapo hali haikuwa shwari kwa muda wa dk 30 baada ya kipenga cha mwisho wa mchezo.
Polisi wakiwapandia washabiki jukwaani hili kuwaadabisha kutoka na vurugu hizo uwanjani hapo
Chupa za maji hiyo wakirushiwa wachezaji wa Equatorial Guinea kutoka kwa washabiki wenye jaziba baada ya timu yao kukubali kipigo.
Helicopter ikizunguka eneo la uwanja kujaribu kuzima vurugu hizo baada ya kipenga cha mwisho 
Hapakutosha uwanjani hapo baada ya wenyeji kukubali kipigo cha bao tatu kwa kibuyu kutoka kwa vijana wa Kighan

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...