Pages

February 11, 2015

Dk Mwakyembe: Hatutazuia magari ya kitalii toka nchi jirani

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Harrison Mwakyembe (katikati) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kushoto ni Katibu mkuu wa Wizara hiyo Joyce Mapunjo na kulia ni Naibu waziri wa Wizara hiyo  Dr. Juma Abdulla Saadala. Picha na Emanuel Herman
 
Na Laura paul,mwananchi
Akizungumza na waandishi wa hahabari jijini Dar es Salaam leo, Dk. Mwakyembe  amesema serikali ya Kenya wameenda kinyume na mkataba wa mwaka 1985 kwa kuvihusisha viwanja vya ndege kuwa sehemu ya vivutio vya utalii jambo lililopelekea kukatazwa kwa magari ya Kitalii yaliyo sajiliwa Tanzania kuingia uwanja wa ndege wa Jomo Kenyata.

Dar es salaam. Waziri Ushirikiano wa Afrika Mashariki  Dk Harison Mwakyembe amesema Tanzania haitazuia magari ya Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki au Nchi nyingine kuingia katika viwanja vyake vya ndege kuleta au kuchukua Watalii wanaopitia katika viwanja hivyo na kwenda katika nchi zao.
Akizungumza na waandishi wa hahabari jijini Dar es Salaam leo, Dk. Mwakyembe  amesema serikali ya Kenya wameenda kinyume na mkataba wa mwaka 1985 kwa kuvihusisha viwanja vya ndege kuwa sehemu ya vivutio vya utalii jambo lililopelekea kukatazwa kwa magari ya Kitalii yaliyo sajiliwa Tanzania kuingia uwanja wa ndege wa Jomo Kenyata.
Dk Mwakyembe amesema  Waziri wa Maliasili na Utalii tayari ameshafanya mazungumzo na Waziri wa Maliasili na Utalii Kenya katikati ya mwezi Januari  ,2015 lengo la kikao hicho ilikuwa ni kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa kukatazwa kwa maghari katika uwanja wa ndege wa Kenya
 “Suala la kurekebisha mkataba ulioingizwa na nchi hizi mbili kwa hiari miaka 30 iliyopita si jepesi, linahitaja mjadala mrefu utakaohusisha taasisi mbalimbali. Hata hivyo vyombo husika vinafanyia kazi suala hilo,amesema Dk Mwakyembe
Amesema Tanzania itachukua hatua ya kuwafahamisha Watalii na wageni wote wenye nia ya kutembelea vivutio vya kitalii vya Tanzania kutumia viwanja vingine vya ndege ili kuepusha kadhia na gharama zisizo za lazima.
Dk Mwakyembe aliongeza kuwa  suala la Magari ya Tanzania kukatazwa kuingia kwenye kiwanja cha Jomo Kenyatta nchini Kenya halitakiwi kabisa kurudisha mahusiano mema miongoni mwa nchi hizi mbili.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...