Pages

October 31, 2014

TABATA FC YAINGIA ROBO FAINALI YA LIGI YA DK. MWAKA SPORTS EXTRA NDONDO CUP BAADA YA KUIFUNGA SIFA POLITAN KWA PENALTI 4-3

 Wachezaji wa timu za Boom FC na Vijana ya Ilala wakisalimiana kabla ya mchezo wao wa hatua ya 16 Bora ya michuano ya Dk. Mwaka Sports Extra Ndondo Cup 2014 uliofanyika katika Uwanja wa Shule ya Sekondari ya Benjamini Mkapa jijini Dar es Salaam. Timu hizo zilitoka sare ya bila kufungana.
 Kikosi cha timu ya Vijana ya Ilala kikiwa katika picha ya pamoja kabla ya mchezo wao na Boom FC katika Uwanja wa Shule ya Sekondari ya Benjamini Mkapa jijini Dar es Salaam.
Kikosi cha timu ya Boom FC kikiwa katika picha ya pamoja.
 Mashabiki wa timu ya Boom FC, wakipiga ngoma wakati timu yao ikicheza na Vijana ya Ilala.

Mshambuliaji wa timu ya Vijana Ilala, Matola Selemani, kushoto akiwania mpira na winga wa timu ya Boom FC, Nambongo Hussein katika mchezo wa Ligi ya Dk. Mwaka Sports Extra Ndondo Cup.
Mshambuliaji wa timu ya Boom FC,Issac Tesha (katikati) akijaribu kufunga  bao katika Ligi ya Dk. Mwaka Sports Extra Ndondo Cup 
Winga wa timu ya Boom FC, akiwatoka mabeki wa timu ya Vijana ya Ilala katika mchezo wa Ligi ya Dk. Mwaka Sports Extra Ndondo Cup. 
Beki wa timu ya Vijana Ilala Ramadhani Yasini, (kushoto) akiwania mpira na mshambuliaji wa timu ya Boom Ally Kondo, katika Ligi ya Dk. Mwaka Sports Extra Ndondo Cup.     
Baadhi ya wadau wa  Soka wakifuatilia mechi kati ya Tabata FC na Sifa Politan kwenye Uwanja wa Bandari.  
Kiungo mshambuliaji wa timu ya Sifa Politan, Mathayo Edward (kulia) akitafuta mbinu za kuwatoka mabeki wa timu ya Tabata FC, katika Ligi ya Dk. Mwaka Sports Extra Ndondo Cup mechi iliyochezwa katika Uwanja wa Bandari Dar es Salaam. Tabata ilishinda kwa Penati 4-3.    
 
 Mashabiki wa timu ya Tabata FC wakishangilia ushindi wa timu yao baada ya kuifunga Sifa Politan kwa mikwaju ya penalti 4-3.
 Kipa wa Sifa Politan akiruka bila mafanikio kujaribu kuokoa penalti iliyopigwa na Kudura Shaban wa Tabata FC. 
Heka Heka katika lango la timu ya BOOM FC.
 
Wadau wa Soka wakifuatilia pambano la Sifa Politan na Tabata FC kwenye Uwanja wa Bandari.
 Mashabiki  soka wakifuatilia pambano la Sifa Politan na Tabata FC kwenye Uwanja wa Bandari.
 Mashabiki wa timu ya Tabata FC wakishangilia ushindi wa timu yao baada ya kuifunga Sifa Politan kwa mikwaju ya penalti 4-3.
Mashabiki wa timu ya Tabata FC wakishangilia ushindi wa timu yao baada ya kuifunga Sifa Politan kwa mikwaju ya penalti 4-3.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...