Pages

October 30, 2014

ANGALIA PICHA AJALI MBAYA ILIYOTOKEA ARUSHA JANA

Simanzi zimetanda jiji la Arusha baada ya watu zaidi ya 10 kufariki dunia  katika ajali iliyotokea eneo la Tengeru. Akiongea na mwandishi wetu mmoja ya mashuhuda aliyefika eneo la tukio na hospitali ya Mount Meru amesema ajali ilitokea majira ya saa kumi jioni huko maeneo ya Sadc-Kwa Fundi  iliyohusisha gari la abiria aina ya Hiace linalobeba watu toka Usa-River kwenda Arusha mjini na Lori la mafuta.Aliongeza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa dereva wa hiace (gari la abiria) iliyokuwa ikijaribu kupita magari mengine ndiyo akakutana uso kwa uso na lori hilo. Habari kamili zitawajia punde. 









No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...