Pages

August 24, 2014

SHULE YAKABILIWA NA UKOSEFU WA BWALO

Wanafunziwa Shule ya Msingi Levolosi iliyopo jijini Arusha wakisoma shairi katika uzinduzi wa jiko la kupikia ambalo limejengwa kwa  msaada na mfanyabiashara, Daniel Materi kwa gharama ya  sh milioni 23.



Na mwandishi wetu,Arusha
Shule ya Msingi Levolosi inakabiliwana na changamoto ya ukosefu wa bwalo la wanafunzi  kulia chakula  nakulazimika kupata huduma ya uji wakiwa madarasani au wakati mwingine nje mazingira ambayo si mazuri kiafya.


Mkuu wa Shule ya Msingi Levolosi, Elisante Kaaya amesema kuwa wamekua wakikosa sehemu maalumu ya wanafunzi kujipatia chakula na kueleza kuwa changamoto nyingine wanazokutana nazo ni pamoja na ukosefu wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia Teknolijia ya habari na mawasiliano(Tehama).


Akisoma taarifa ya Shule hiyo katika uzinduzi  wa jiko la shule, lilojengwa kwa msaada wa mfanyabiashara Daniel Materi  ikiwa ni njia mojawapo ya kuunga mkono juhudi za kufanikisha mpango wa chakula mashuleni.


Elisante Kaaya amewapongeza wadau wote waliojitoa kuwezesha watoto wa shule hiyo kupata uji kwani mwakani wanatarajia watoto watapata huduma ya chakula cha mchana shuleni hapo.


Mbunge wa Simanjiro mkoa wa Manyara, Christopher Ole Sendeka amesema kuwa  ni jukumu la jamii kujitoa kusaidia watoto waweze kusoma na kuzingatia taaluma ili waweze kufaulu.


Hata hivyo mkuu wa wilaya ya Arusha, John Mongela alihimiza  juhudi nzuri zilizofanywa na mfanyabiashara huyo ziigwe na wengine kwani serikali pekee yake haitaweza kutoa zote kutokana na kukabiliwa na majukumu mengi.


Daniel amesema kuwa msaada huo ni mchango wa kuisaidia jamii inayomzunguka hususani katika masuala ya elimu ambayo ni muhimu kwa jamii yetu.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...