Pages

July 25, 2014

MKUU WA MKOA WA MOROGORO AFUNGUA WARSHA YA UHIFADHI IKISHIRIKISHA TANAPA NA BAADHI YA WADAU WA UHIFADHI

Viongozi wa ngazi ya juu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama nchini kwa mikoa iliyo jirani na Hifadhi za Taifa wanakutana Nashera Hotel kujadili ushirikiano baina yao na Hifadhi za Taifa,(TANAPA) katika kupambana na uhalifu unaolenga Maliasili.


Mgeni Rasmi katika Warsha ya Mashirikiano kati ya TANAPA na Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Mkuu wa Mkoa wa Mororgoro Joel Bendera (wa tatu toka kulia) akiwa na viongozi wengine,toka kushoto ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro SACP, Leonard Paul, Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Elias Tarimo, Mkurugenzi Mkuu TANAPA, Allan Kijazi. Wengine baada ya RC Bendera ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Wanyamapori, Paul Sarakikya na mwisho ni Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Said Amanzi.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Joel Bendera akifungua warsha ya Mashirikiano baina ya Vyombo vya Ulinzi na Usalama kwa mikoa iliyo jirani na Hifadhi za Taifa .
Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi za Taifa, (TANAPA) Allan Kijazi akitoa salamu zake wakati wa ufunguzi wa Warsha ya  Mashirikiano kwa Vyombo vya Ulinzi na Usalama kwa mikoa inayopakana na Hifadhi za Taifa. Mkutano unaofanyika katika Hoteli ya Nashera mkoani Morogoro.
Mmoja wa washiriki katika Warsha ya Mashirikiano baina ya Vyombo vya Ulinzi na Usalama na TANAPA,  Mrakibu wa Polisi, Mary Lugola akitoa neno la shukrani kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera mara baada ya kufungua warsha ya viongozi hao .
Baadhi ya washiriki katika warsha hiyo wakifuatilia hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera alipokuwa akifungua warsha hiyo.
Baadhi ya waandishi wa habari toka vyombo mbalimbali vya habari nchini wakichukua matukio muhimu wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo.
Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Milima ya Udzungwa, Vitalis Uruka akitoa mada juu ya Changamaoto za Uhifadhi katika Kanda ya Kusini na hali halisi.
Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Tarangire Stephen Qoli akitoa mada juu ya Changamaoto za Uhifadhi katika Kanda ya Kaskazini na hali halisi.
Meneja Mawasiliano, TANAPA Pascal Shelutete akitoa mada ya Utaratibu wa kutoa Taarifa kwa Umma juu ya masuala ya Ulinzi na Usalama wa Maliasili na Watalii.
Mshiriki wa warsha hiyo, Franco Kibona akichangia mada katika warsha hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Elias Tarimo akichangia mada wakati wa warsha hiyo.
Mshiriki Abdulla Suleiman akichangia mada katika warsha hiyo.
Mshiriki Faustine Masalu akichangia mada katika warsha hiyo.
Mkurugenzi Mkuu TANAPA, Allan Kijazi akichagia mada katika warsha hiyo.
Washiriki wa warsha hiyo wakiwa katika picha ya pamoja.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA, Allan Kijazi pamoja na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro SACP, Leonard Paul mara baada ya ufunguzi wa warsha hiyo.Na Dixon Busagaga wa globu ya jamii kanda ya kaskazini aliyeko Morogoro.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...