Pages

April 25, 2014

GODBLESS LEMA KUUNGURUMA LEO KWA WAPIGAKURA WAKE



Baadhi ya Madiwani wa halmashauri ya Jiji la Arusha kupitia Chadema wakizungumza na wananchi hivi karibuni.
Arusha. Hatimaye Jeshi la Polisi wilayani Arusha limeruhusu mikutano ya hadhara ya Mbunge wa Arusha (Chadema), Godbless Lema baada ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magessa Mulongo kuingilia kati.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Lebaratus Sabas alithibitisha jana kuruhusiwa kwa mikutano hiyo licha ya kuizuia awali baada ya kujiridhisha na hali ya kiusalama.
Uamuzi wa polisi unakuja baada ya Lema kushikilia msimamo wa kuendelea na mikutano akisema sababu zilizotolewa na polisi hazikuwa na mashiko.
Polisi ilizuia mikutano ya Lema aliyetoa taarifa Aprili 17, mwaka huu, baada ya CCM kuomba kufanya mikutano siku mbili baada ya taarifa yake, ikitaja siku na maeneo hayohayo ya mbunge huyo.
Awali, Mkuu wa Polisi Wilaya (OCD) Arusha, Giles Muroto aliyezuia mikutano hiyo, pia alitaja hofu ya mlipuko wa bomu kama sababu nyingine ya kuzuia mikutano ya Lema.
Jana asubuhi, Mkuu wa Mkoa wa Arusha alikaririwa na kituo cha Radio 5 cha Arusha akiliagiza jeshi la polisi kutathmini hali ya usalama na kumruhusu Lema kutimiza wajibu wake wa kibunge kwa kukutana na wapiga kura wake kupitia mikutano ya hadhara.
“Pamoja na polisi kutaja sababu za kuzuia mikutano ya hadhara Arusha, tutawashauri , wafanye tathmini kuruhusu mikutano ya mbunge ili atimize wajibu wake wa kibunge,” alikaririwa Mulongo.
Hata hivyo, Mulongo alikiri Jiji la Arusha kuwa katika hali tete na hofu kutokana na tukio la mlipuko wa bomu kwenye Baa ya Arusha Night Park, Aprili 13, mwaka huu.


No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...