Pages

July 10, 2013

KAMPUNI YA UJENZI YA A.E.BUILDING AND CIVIL ENGENEERING LTD YAJENDA DARAJA LA KISASA LEMARA

 
 Mkurugenzi wa Kampuni ya   A.E.Building and Civil Enginering Limited ya Arusha,Ally Swai akizungumza na waandishi wa habari. 



 
Mafundi wakiendelea na ujenzi
Arusha.
Wananchi wa Kata ya Lemara,jijini Arusha  wataondokana na kero iliyokua ikiwasumbua kwa muda mrefu hasa wakati wa mvua baada ya daraja jipya la Kikwakwaru B linalojengwa kwa gharama za Mfuko wa  barabara kukamilika mwezi huu.
Akizungumzia maendeleo ya ujenzi huo,Mhandisi wa Jiji la Arusha, Elias Biromo alisema  ujenzi umekamilika kwa asilimia 60 na linajengwa kwa kiwango walichokubalina na kampuni ya ujenzi ya A.E.Building and Civil Enginering Limited ya Arusha kwa gharama ya Sh 157 milioni.
Amesema daraja hilo litakua ni ukombozi kwa wananchi wa Kata hiyo na Kata jirani ambao wamekua wakipata shida kutumia daraja ambalo lilikua haliwezi kuhimili idadi ya magari na kuwa mpango ni kuunganisha barabara hiyo  kutoka Njiro hadi Kata ya Sombetini.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa kampuni inayojenga daraja hilo,Ally Swai amesema ujenzi ulichelewa kutokana na mvua zilizosimamisha ujenzi kwa muda na upungufu wa vitendea kazi ambayo ilikua ni  changamoto katika kazi hiyo.
“Nawataka wananchi wavumilie ujenzi wa daraja unahitaji umakini mkubwa na utakamilika muda si mrefu,kumekua na maneno ya kisiasa ambayo lengo lake sio zuri jambo la msingi ni daraja likamilike liweze kurahisisha mawasiliano na wananchi wafanye biashara zao,”alisema Swai
Amesema wakati mwingine wanasiasa wamekua kikwazo katika kazi za kitaalamu na kusababisha migongano isiyo ya msingi katika jamii wakati wananchi wanahitaji miundombinu ili kuwawezesha kujiletea maendeleo.
 
 
 
 

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...