Pages

March 29, 2017

Solly Mahlangu kutoka nchini Afrika kusini athibitisha kushiriki tamasha la Pasaka jijini Dar


MWIMBAJI wa kimataifa wa nyimbo za injili, Pastor Solly Mahalangu kutoka nchini Afrika Kusini, amethibitisha kushiriki Tamasha la Pasaka linaloadhimisha miaka 17 tangu kuasisiwa kwake mwaka 2000 chini ya uratibu wa kampuni ya Msama Promotions.

Solly ambaye amekuwa king’ara vilivyo katika muziki wa injili kama mwimbaji anayejipambanua na wengine kama mchangamshaji zaidi jukwaani, pia ni kiongozi wa kanisa nchini Afrika Kusini , hivyo kuenfesha huduma zote mbili kila moja kwa wakati wake.

Alex Msama, Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha hilo litakalozinduliwa April 16, mwaka huu katika Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam kabla ya kuelekea katika mikoa mingine mitano, alisema jana kwamba mwimbaji huyo amethibitisha kushiriki tukio hilo lenye kubeba hadhi na vionjo vya kimataifa.

“Nikiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka, nina furaha kubwa kusema kuwa mwimbaji wa kimataifa wa nyimbo za injili kutoka nchini Afrika Kusini, amethibitisha kushiriki tamasha la Pasaka la mwaka huu litakalofanyika katika mikoa sita ikiwemo Dar es Salaam,” alisema.

Alisema ujio wa Mahlangu katika tamasha hilo, kunafanya maandalizi ya Tamasha hilo yazidi kuimarika kutokana na umaarufu wa mwimbaji huyo anayesifika ndani na nje ya Afrika Kusini kwa huduma ya uimbaji wa nyimbo zenye ujumbe wa kuvutia wengi na kuchangamsha jukwaa.

Msama alisema kwa vile si mara ya kwanza kwa Mahlangu kushiriki Tamasha la Pasaka, wadau na wapenzi wa Tasmaha hilo wajitokeze kwa wingi kuja kufaidi Baraka za Mungu kupitia ujumbe wa Neno la Mungu kutoka kwa mwimbaji huyo na wengine kibao akiwemo malkia wa muziki wa injili Afrika Mashariki, Rose Muhando.

Alisema Mahlangu ambaye atakuwa na kundi lake, atashirikiana na waimbaji wengine walitangazwa tayari ambao tayari wapo katika maandalizi ya nguvu kwa lengo la kutoa huduma bora siku hiyo ya uzinduzi wa Tamasha hilo lenye kubeba maudhui ya kueneza ujumbe wa neno la Mungu na sehemu ya mapato kusaidi makundi maalumu.

Msama alisema Tamasha la mwaka huu litabeba uzinduzi wa albamu mbili; moja ya Muhando inayoitwa Jitenge na Ruth pamoja na albamu mpya ya Kwaya ya Kinondoni Revival ya jijini Dar es Salaam, iitwayo ‘Ngome Imeanguka.’

Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Alex Msama, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kuhusu maandalizi ya tamasha hilo litakalofanyika Aprili 16 kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. 
Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Alex Msama, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kuhusu maandalizi ya tamasha hilo litakalofanyika Aprili 16 kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. 
Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Alex Msama, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, kuhusu maandalizi ya tamasha hilo litakalofanyika Aprili 16 kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...